Ratiba ya Juma Linaloanza Septemba 7
JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 7
Wimbo 3 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 30 ¶1-9 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 12-15 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Wafalme 13:12-19 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Maana ya Dhambi—td 3A (Dak. 5)
Na. 3: Vitabu vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Vina Ujumbe Gani?—igw uku. 31 (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: “Mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Yehova.” —Yos. 24:15.
Dak. 10: Tulipata Matokeo Gani? Mazungumzo. Waombe wahubiri waeleze jinsi walivyofaidika kwa kutumia mapendekezo yaliyo katika makala “Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuwazoeza Wapya.” Waombe wahubiri wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo.
Dak. 10: Je, Kuhudhuria Mikutano ya Kutaniko ni Desturi ya Familia Yenu? Hotuba inayotegemea Waebrania 10:24, 25. Hoji familia yenye watoto. Kichwa cha familia anahakikishaje kwamba mikutano inapewa nafasi ya kwanza? Kila mmoja anafanya jitihada gani ili kuhakikisha kwamba familia yote inahudhuria mikutano kwa ukawaida? Wanatayarisha maelezo yao wakati gani? Wanadhabihu mambo gani ili wahudhurie mikutano? Malizia kwa kuwatia moyo wote wahudhurie na kushiriki mikutano kwa ukawaida.
Dak. 10: Je, Unaweza Kupanda Mbegu za kweli ya Biblia kwa Watu Wako wa Ukoo? (Mdo. 10:24, 33, 48) Mazungumzo yanayotegemea Kitabu cha Mwaka—2015, ukurasa wa 87, fungu la 1-2; na ukurasa wa 90, fungu la 1-3. Waombe wasikilizaji waeleze mambo waliyojifunza. Ikiwa Kitabu cha Mwaka 2015 hakipatikani, tumia habari iliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 1997, ukurasa wa 1, yenye kichwa “Vipi Jamaa Zako?”
Wimbo 118 na Sala