Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 90-uku. 94 fu. 3
  • “Siku Moja Tutawapata”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Siku Moja Tutawapata”
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • “Siku Moja Tutawapata”
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 90-uku. 94 fu. 3

JAMHURI YA DOMINIKA

“Tutawapata”

“Siku Moja Tutawapata”

Picha katika ukurasa wa 91

Mwaka wa 1935 hivi, Pablo González kutoka katika eneo la Bonde la Cibao, alianza kusoma Biblia. Alishirikiana kwa muda mfupi na kikundi cha Kiprotestanti, lakini aliacha baada ya kuona matendo yao hayapatani na mambo aliyosoma kwenye Maandiko. Hata hivyo, aliendelea kujifunza peke yake Neno la Mungu na alianza kuwaambia wengine mambo aliyokuwa akijifunza, aliiambia kwanza familia na jirani zake, kisha wengine katika maeneo ya karibu. Aliuza shamba na ng’ombe wake na kutumia pesa hizo kugharimia safari zake kwa ajili ya huduma.

Kufikia mwaka wa 1942, Pablo alikuwa akitembelea karibu familia 200 katika maeneo mbalimbali na kufanya mikutano kwa ukawaida, hata ingawa hakuwa amekutana na Mashahidi wa Yehova. Aliwahimiza watu wajifunze Biblia na waishi kupatana na yale waliyojifunza. Wengi walizingatia yale aliyosema na wakaacha kuvuta sigara na kuacha zoea la kuoa wake wengi.

Picha katika ukurasa wa 91

Miongoni mwa wale waliosikiliza ujumbe wa Biblia wa Pablo, alikuwa Celeste Rosario. Alikumbuka hivi: “Nilipokuwa na umri wa miaka 17, binamu ya mama yangu, Negro Jiménez, alikuwa mshiriki wa kikundi kimoja kilichoongozwa na Pablo González. Alitembelea familia yetu na kutusomea baadhi ya maandiko ya Biblia, na hilo lilinichochea vya kutosha kuliacha Kanisa Katoliki. Mambo tuliyosikia kanisani yalisomwa kwa Kilatini, lugha ambayo hatukuielewa. Muda mfupi baadaye, Pablo González alitutembelea na kutuimarisha. Alisema hivi: ‘Sisi si waumini wa dini yoyote kati ya hizi tunazozijua, lakini tuna ndugu ulimwenguni pote. Bado hatujui ni akina nani au wanaitwa kwa jina gani, lakini siku moja tutawapata.’”

Pablo alikuwa ameanzisha vikundi vya wanafunzi wa Biblia katika mji wa Los Cacaos Salcedo, Monte Adentro, Salcedo, na Villa Tenares. Mwaka wa 1948, alipokuwa safarini jijini Santiago, aliwaona Mashahidi wawili wakihubiri barabarani, nao wakampa gazeti la Mnara wa Mlinzi. Katika safari nyingine jijini Santiago, dada fulani alimpa Pablo vitabu viwili na kumwalika kwenye Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Alivutiwa sana na mambo aliyosikia katika Ukumbusho huo, hivi kwamba alikata shauri kuwa hatimaye ameipata kweli na wale waliohudhuria mkutano huo ndio watu aliotazamia kuwapata.

Wamishonari waliwatembelea watu ambao Pablo alikuwa akiwafundisha. Katika sehemu moja ambayo Pablo alikuwa akifanyia mikutano, walikuta watu 27 waliokuwa wakiwasubiri kwa hamu. Baadhi yao walisafiri umbali wa kilometa 25 kwa miguu ili kufika sehemu hiyo; na wengine kilometa 50 kwa farasi! Katika sehemu iliyofuata, kulikuwa na watu 78, na sehemu nyingine watu 69 walikusanyika kwa ajili ya mkutano.

Pablo aliwapa wamishonari majina ya watu 150 hivi waliopenda kujifunza. Watu hao wanyenyekevu na waliompenda Mungu tayari walikuwa wakijifunza na kufuata kanuni za Biblia maishani. Walichohitaji kilikuwa tengenezo na mwongozo. Celeste alisema hivi: “Wamishonari walitutembelea na tukafanya mkutano. Mipango ilifanywa ili kuwe na ubatizo. Nilikuwa wa kwanza kubatizwa katika familia yetu. Katika mkutano mwingine, mama yangu, Fidelia Jiménez, na dada yangu, Carmen, wakabatizwa pia.”

Kusanyiko la kwanza la mzunguko katika Jamhuri ya Dominika, ambalo lilifanywa jijini Santiago, Septemba 23-25, 1949, lilichochea zaidi kazi ya kuhubiri. Watu wengi wenye hamu ya kujifunza walikuja, na jumla ya watu 260 walisikiliza hotuba ya watu wote siku ya Jumapili. Watu 28 wakabatizwa. Kusanyiko hilo la siku tatu liliwathibitishia watu wengi kwamba Mashahidi wa Yehova ndio kikundi kinachofanya mapenzi ya Mungu.

Historia ya Awali

  1. 1945

    Wamishonari Lennart na Virginia Johnson wawasili

    Picha katika ukurasa wa 92
  2. 1946

    Ziara ya Ndugu Knorr na Ndugu Franz

    Picha katika ukurasa wa 92
  3. 1949

    Kusanyiko la kwanza la mzunguko

    Watu 28 wabatizwa kwenye Mto North Yaque

    Picha katika ukurasa wa 93
  4. 1950

    Mashahidi wa Yehova wapigwa marufuku

    Picha katika ukurasa wa 93
    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki