Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/15 uku. 3
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 10/15 uku. 3

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Oktoba 26, 2015.

  1. Simulizi lililo katika 2 Wafalme 13:18, 19 linaonyeshaje umuhimu wa kumtumikia Yehova kwa bidii na kwa moyo wote? [Sept. 7, w10 4/15 uku. 26-27 fu. 11]

  2. Ni nani aliyekuwa anatawala Israeli wakati Yona alipotumikia akiwa nabii? Tunajifunza jambo gani zuri kuhusu huduma ya Yona kutokana na yale yalioandikwa katika 2 Wafalme 14:23-25? [Sept. 7, w09 1/1 uku. 25 fu. 4]

  3. Ahazi alionyeshaje kwamba hakutegemea neno la Mungu lililosemwa kupitia nabii Isaya, na tunaweza kujiuliza swali gani tunapofanya maamuzi mazito? (2 Fal. 16:7) [Sept. 14, w13 11/15 uku. 17 fu. 5]

  4. Ni mbinu gani iliyotumiwa na Rabshake ambayo inatumiwa pia na adui za watu wa Mungu leo, na ni sifa gani inayoweza kutusaidia kukataa mawazo ya wapinzani? (2 Fal. 18:22, 25) [Sept. 14, w10 7/15 uku. 13 fu. 3-4]

  5. Tunaposoma na kujifunza Biblia, tunawezaje kufaidika na mfano wa Yosia wa unyenyekevu? (2 Fal. 22:19, 20) [Sept. 21, w00 3/1 uku. 30 fu. 2]

  6. Uchimbuaji wa vitu vya kale umethibitishaje kwamba wafalme wawili wanaotajwa katika 2 Wafalme 25:27-30 walikuwako? [Sept. 28, w12 6/1 uku. 5 fu. 2-3]

  7. Yabesi alimwomba Yehova mambo gani matatu, na hilo linatufundisha nini kuhusu sala? (1 Nya. 4:9, 10) [Okt. 5, w10 10/1 uku. 23]

  8. Matokeo ya vita vinavyosimuliwa katika 1 Mambo ya Nyakati 5:18-22 yanawezaje kutuimarisha kuendelea kupigana vita vyetu vya kiroho kwa ujasiri? [Okt. 12, w05 10/1 uku. 9 fu. 7]

  9. Kwa nini Daudi alifahamu na kutii kusudi la sheria ya Yehova kuhusu utakatifu wa damu? Mfano huo wa Daudi unapaswa kutuchochea kufanya nini? (1 Nya. 11:17-19) [Okt. 19, w12 11/15 uku. 6-7 fu. 12-14]

  10. Daudi alikosa kufanya nini mara ya kwanza alipojaribu kuleta sanduku la agano jijini Yerusalemu? Tunajifunza somo gani muhimu kutokana na kisa hicho? (1 Nya. 15:13) [Okt. 26, w03 5/1 uku. 10-11 fu. 11-13]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki