Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Oktoba 26, 2015.
Simulizi lililo katika 2 Wafalme 13:18, 19 linaonyeshaje umuhimu wa kumtumikia Yehova kwa bidii na kwa moyo wote? [Sept. 7, w10 4/15 uku. 26-27 fu. 11]
Ni nani aliyekuwa anatawala Israeli wakati Yona alipotumikia akiwa nabii? Tunajifunza jambo gani zuri kuhusu huduma ya Yona kutokana na yale yalioandikwa katika 2 Wafalme 14:23-25? [Sept. 7, w09 1/1 uku. 25 fu. 4]
Ahazi alionyeshaje kwamba hakutegemea neno la Mungu lililosemwa kupitia nabii Isaya, na tunaweza kujiuliza swali gani tunapofanya maamuzi mazito? (2 Fal. 16:7) [Sept. 14, w13 11/15 uku. 17 fu. 5]
Ni mbinu gani iliyotumiwa na Rabshake ambayo inatumiwa pia na adui za watu wa Mungu leo, na ni sifa gani inayoweza kutusaidia kukataa mawazo ya wapinzani? (2 Fal. 18:22, 25) [Sept. 14, w10 7/15 uku. 13 fu. 3-4]
Tunaposoma na kujifunza Biblia, tunawezaje kufaidika na mfano wa Yosia wa unyenyekevu? (2 Fal. 22:19, 20) [Sept. 21, w00 3/1 uku. 30 fu. 2]
Uchimbuaji wa vitu vya kale umethibitishaje kwamba wafalme wawili wanaotajwa katika 2 Wafalme 25:27-30 walikuwako? [Sept. 28, w12 6/1 uku. 5 fu. 2-3]
Yabesi alimwomba Yehova mambo gani matatu, na hilo linatufundisha nini kuhusu sala? (1 Nya. 4:9, 10) [Okt. 5, w10 10/1 uku. 23]
Matokeo ya vita vinavyosimuliwa katika 1 Mambo ya Nyakati 5:18-22 yanawezaje kutuimarisha kuendelea kupigana vita vyetu vya kiroho kwa ujasiri? [Okt. 12, w05 10/1 uku. 9 fu. 7]
Kwa nini Daudi alifahamu na kutii kusudi la sheria ya Yehova kuhusu utakatifu wa damu? Mfano huo wa Daudi unapaswa kutuchochea kufanya nini? (1 Nya. 11:17-19) [Okt. 19, w12 11/15 uku. 6-7 fu. 12-14]
Daudi alikosa kufanya nini mara ya kwanza alipojaribu kuleta sanduku la agano jijini Yerusalemu? Tunajifunza somo gani muhimu kutokana na kisa hicho? (1 Nya. 15:13) [Okt. 26, w03 5/1 uku. 10-11 fu. 11-13]