Je, Neno la Mungu Linaongoza Maisha Yako Kila Siku?
Kusoma Biblia kila siku kunaweza kutusaidia ‘kutia mizizi’ na “kuimarishwa katika imani.” (Kol. 2:6, 7) Hata hivyo, ili Neno la Mungu liongoze maisha yetu, lazima tutafakari na kutumia kanuni zake. (Ebr. 4:12; Yak. 1:22-25) Andiko la Yoshua 1:8 linaonyesha hatua tatu zenye matokeo: (1) Soma Neno la Mungu “mchana na usiku.” (2) Soma “kwa sauti ya chini,” yaani, usome kwa mwendo utakaokuruhusu kutafakari na kuwazia mandhari na hali zilizokuwepo. (3) Jitahidi kutumia “yote ambayo yameandikwa ndani yake.” Kufuata madokezo hayo kutatusaidia ‘tufanikiwe’ na ‘tutende kwa hekima’ katika maisha yetu ya kila siku.