Ratiba ya Juma Linaloanza Oktoba 26
JUMA LINALOANZA OKTOBA 26
Wimbo 15 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
ia sura ya 1 ¶1-13 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 12-15 (Dak. 8)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: ‘Tia mizizi’ na “kuimarishwa katika imani.”—Kol. 2:6, 7.
Dak. 10: Machapisho Yatakayotolewa Mwezi wa Novemba. Mazungumzo. Watie moyo wahubiri watoe trakti na kitabu Biblia Inafundisha katika utumishi wa shambani. Zungumzia kwa ufupi habari muhimu zinazopatikana kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 2014 katika makala yenye kichwa “Muundo wa Kuvutia wa Trakti Mpya!” Tia ndani onyesho linalofaa katika eneo lenu.
Dak. 20: “Je, Neno la Mungu Linaongoza Maisha Yako Kila Siku?” Hotuba. Baada ya utangulizi mfupi, sikilizeni drama ya usomaji wa Biblia katika Tovuti ya jw.org/sw yenye kichwa “Usife Moyo Unaporekebishwa na Yehova!” Kazia jinsi kutafakari Neno la Mungu kunavyoweza kutusaidia kupata kanuni tunazoweza kutumia. Malizia hotuba kwa kuwatia moyo wote wanufaike na drama za usomaji wa Biblia zinazopatikana katika jw.org/sw. Maeneo ambayo haiwezekani kutumia tovuti hiyo, mwombe ndugu anayesoma vizuri ajitayarishe mapema kusoma Waebrania 12:1-12, na uonyeshe jinsi ambavyo kutafakari kuhusu sehemu hiyo kunavyoweza kutusaidia tusife moyo tunaporekebishwa na faida tutakazopata kwa kufuata shauri.
Wimbo 113 na Sala