Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuwazoeza Wanafunzi wa Biblia Wawe na Mazoea Mazuri ya Kujifunza
Kwa Nini Ni Muhimu: Wanafunzi wa Biblia wanahitaji mafundisho ya msingi ya Neno la Mungu, lakini ili wafanye maendeleo kufikia ukomavu wa kiroho ni lazima walishe akili na moyo wao mengi zaidi ya mambo hayo. (Ebr. 5:12–6:1) Kujifunza kunahitaji jitihada. Kunatia ndani kuhusianisha mambo mapya tunayojifunza na yale ambayo tayari tunajua, na kutambua thamani ya mambo hayo. (Met. 2:1-6) Kujifunza kufanya utafiti kutamsaidia mwanafunzi kujibu maswali ya Biblia kwa kutumia machapisho yetu ya Kikristo. Kujitahidi kutumia mambo wanayojifunza kutawasaidia kuvumilia majaribu watakayokabili katika maisha yao ya Kikristo.—Luka 6:47, 48.
Jaribu Kutumia Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Mnapomaliza kuzungumzia kichwa kidogo au sura, mwombe mwanafunzi wako wa Biblia aeleze kwa maneno machache mambo aliyojifunza. Ikiwa huna mwanafunzi wa Biblia, jizoeze kueleza kwa ufupi fungu fulani la maneno katika Biblia au katika gazeti la Mnara wa Mlinzi ili kuboresha uwezo wako wa kusoma na kuelewa.