Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 7
JUMA LINALOANZA DESEMBA 7
Wimbo 86 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
ia sura ya 4 ¶1-15, sanduku kwenye uku. 39 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Mambo ya Nyakati 10-14 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Mambo ya Nyakati 13:13-22 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Roho Takatifu Si Mtu—td 39D (Dak. 5)
Na. 3: “Kaisari” Maana Yake Nini? (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: “Lazima tuingie katika Ufalme wa Mungu kupitia dhiki nyingi.” —Matendo 14:22.
Dak. 10: “Lazima Tuingie Katika Ufalme wa Mungu Kupitia Dhiki Nyingi.” Hotuba inayotegemea kichwa cha mwezi huu. Soma na uzungumzie Matendo 14:21, 22; na 1 Petro 4:12-14. (Ona gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 2014, uku. 13, fu. 3-6.) Pitia baadhi ya sehemu za Mkutano wa Utumishi, na uzungumzie jinsi zinavyohusiana na kichwa cha mwezi huu. Watie moyo watu wote watazame video ‘Tembea kwa Imani, Si kwa Kuona’ ili wajitayarishe kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi wa juma litakalofuata.
Dak. 10: Unapaswa Kujibu kwa Njia Gani? (Kol. 4:6) Hotuba inayotegemea kitabu Shule ya Huduma ukurasa wa 69, fungu la 1-3. Panga kuwe na maonyesho mawili. Katika onyesho la kwanza, mhubiri anamkatiza kwa njia isiyofaa mwenye nyumba anapoongea kwa ukali, matokeo yanakuwa mabaya. Katika onyesho la pili, baada ya mwenye nyumba kuongea kwa ukali, mhubiri anasikiliza bila kukatiza, kisha baadaye anajibu kwa upole, na matokeo yanakuwa mazuri.
Dak. 10: “Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Habakuki.” Maswali na majibu.
Wimbo 74 na Sala