HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 45-51
Yehova Hataudharau Moyo Uliovunjika
Zaburi ya 51 iliandikwa na Daudi baada ya nabii Nathani kumweleza kuhusu dhambi nzito ya uzinzi aliyofanya na Bath-sheba. Dhamiri ya Daudi ilimsumbua, na akaungama kwa unyenyekevu.—2Sa 12:1-14.
Daudi alitenda dhambi lakini bado angeweza kurudia hali yake nzuri ya kiroho
Kabla ya Daudi kutubu na kuungama dhambi zake, dhamiri yake ilimtaabisha
Alipata maumivu makali sana kwa sababu ya kukosa kibali cha Mungu hivi kwamba alikuwa kama mtu aliyepondwa mifupa
Alitamani kusamehewa, kurudia hali nzuri ya kiroho, na kurudishiwa shangwe aliyokuwa nayo
Alimwomba Yehova kwa unyenyekevu amsaidie kukuza tamaa ya kutii
Alikuwa na uhakika kwamba Mungu angemsamehe