HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 74-78
Kumbuka Matendo ya Yehova
Ni muhimu kutafakari mambo mazuri ambayo Yehova ametufanyia
Kutafakari hutusaidia kuelewa mambo tunayosoma katika Neno la Mungu na kuthamini chakula cha kiroho
Kutafakari kwa kina kumhusu Yehova hutusaidia kukumbuka kazi zake za ajabu na tumaini ambalo ametuahidi
Kazi za Yehova zinatia ndani mambo yafuatayo:
Uumbaji
Kadiri tunavyojifunza kuhusu uumbaji, ndivyo tunavyostaajabishwa na kumheshimu Yehova zaidi
Wanaume waliowekwa rasmi kutanikoni
Tunapaswa kujinyenyekeza kwa wale ambao Yehova amewachagua ili kuongoza
Matendo ya wokovu
Kukumbuka matendo ya Yehova ya wokovu kunaimarisha imani yetu kwamba anataka na ana uwezo wa kuwatunza watumishi wake