Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr16 Julai uku. 1
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2016
  • Vichwa vidogo
  • JULAI 4-10
  • JULAI 18-24
Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2016
mwbr16 Julai uku. 1

Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

JULAI 4-10

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 60-68

“Msifu Yehova, Msikiaji wa Sala”

it-2 668 ¶2

Sala

Wale Ambao Mungu Huwasikiliza. Watu “wote wenye mwili” wanaweza kuja kwa “msikiaji wa sala,” Yehova Mungu. (Zb 65:2; Mdo 15:17) Hata wakati ambapo taifa la Israeli lilikuwa ‘mali binafsi ya Mungu,’ watu aliofanya nao agano, wageni wangeweza kusali kwa Yehova ikiwa walitambua kwamba taifa la Israeli ndicho chombo kilichochaguliwa na Mungu na kwamba hekalu la Yerusalemu ndipo mahali alipochagua kwa ajili ya kumtolea dhabihu. (Kum 9:29; 2Nya 6:32, 33; linganisha Isa 19:22.) Baadaye, kupitia kifo cha Kristo, tofauti kati ya Myahudi na mtu wa mataifa iliondolewa milele. (Efe 2:11-16) Katika nyumba ya Mwitaliano aliyeitwa Kornelio, Petro alitambua kwamba “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.” (Mdo 10:34, 35) Hivyo, kinachoamua ni moyo wa mtu mwenyewe na kile ambacho moyo wake unamchochea kutenda. (Zb 119:145; Omb 3:41) Wale wanaoshika amri za Mungu na kufanya “mambo yanayopendeza machoni pake,” wana uhakika kwamba “masikio” yake yanawasikiliza wao pia.—1Yo 3:22; Zb 10:17; Met 15:8; 1Pe 3:12.

JULAI 18-24

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 74-78

“Kumbuka Matendo ya Yehova”

it-1 1160 ¶7

Unyenyekevu

Wote, wanaume na wanawake, wanapaswa kujitiisha kwa wale wanaoongoza na kumngojea Yehova awaweke rasmi au kuwapa migawo ya madaraka, kwa kuwa yeye ndiye huitoa. (Zb 75:6, 7) Baadhi ya Walawi, wana wa Kora walisema hivi: “Nimechagua kusimama mlangoni pa nyumba ya Mungu wangu badala ya kuzunguka katika mahema ya uovu.” (Zb 84:10) Muda unahitajika ili mtu asitawishe unyenyekevu wa kweli. Maandiko yanapozungumzia sifa za mtu kustahili kuwekwa rasmi kuwa mwangalizi, yanataja kihususa kwamba mtu aliyegeuzwa imani hivi karibuni hapaswi kuwekwa rasmi ili “asije akajivuna kwa kiburi na kuanguka katika hukumu iliyopitishwa juu ya Ibilisi.”—1Ti 3:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki