Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr16 Agosti uku. 1
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2016
  • Vichwa vidogo
  • AGOSTI 22-28
  • AGOSTI 29–SEPTEMBA 4
Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2016
mwbr16 Agosti uku. 1

Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

AGOSTI 22-28

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 857-858

Kujua Kimbele, Kupanga Kimbele

Je, Mungu alipanga mapema kwamba Yuda amsaliti Yesu ili kutimiza unabii?

Usaliti wa Yuda ulitimiza unabii uliotolewa na Mungu na pia ukaonyesha uwezo wa Yehova na wa Mwana wake wa kujua mambo kimbele. (Zb 41:9; 55:12, 13; 109:8; Mdo 1:16-20) Hata hivyo, Mungu hakupanga kimbele kwamba Yuda awe msaliti. Unabii ulitabiri kwamba Yesu angesalitiwa na mmoja wa rafiki zake wa karibu, lakini haukusema kihususa ni nani kati yao ambaye angefanya hivyo. Isitoshe, kanuni za Biblia zinaonyesha wazi kwamba Mungu hawezi kuwa alipanga kimbele matendo ya Yuda. Paulo aliandika kanuni hii ya Mungu inayosema hivi: “Usiweke kamwe mikono yako juu ya mtu yeyote haraka-haraka; wala usiwe mshiriki katika dhambi za wengine; jihifadhi ukiwa safi kiadili.” (1Ti 5:22; linganisha 3:6.) Jambo linaloonyesha wazi kwamba Yesu alitaka kuwachagua wale mitume 12 kwa hekima na kwa njia inayofaa, ni kwamba alitumia usiku mzima akisali kwa Baba yake kabla ya kumjulisha mtu yeyote uamuzi wake. (Lu 6:12-16) Ikiwa Yuda alikuwa amepangiwa kimbele kuwa msaliti, hilo halingepatana na maagizo na mwongozo wa Mungu, na kulingana na kanuni hiyo ya kimaandiko, Mungu angekuwa mshiriki katika dhambi ambazo mtu huyo alitenda.

Hivyo, ni wazi kwamba Yuda alipochaguliwa kuwa mtume, moyo wake haukuwa na mwelekeo wowote wa usaliti. Yeye aliruhusu ‘mzizi wenye sumu uchipuke’ na kumtia unajisi, na kusababisha apotoke na kukubali kuongozwa na Ibilisi katika wizi na hila, badala ya kukubali mwongozo wa Mungu. (Ebr 12:14, 15; Yoh 13:2; Mdo 1:24, 25; Yak 1:14, 15) Kadiri muda ulivyosonga, upotovu huo ulifikia kiwango kibaya, hivi kwamba Yesu mwenyewe angeweza kusoma moyo wa Yuda na kutabiri kwamba angemsaliti.​—Yoh 13:10, 11.

Ni kweli kwamba simulizi la Yohana 6:64 linaonyesha kwamba pindi ile baadhi ya wanafunzi walikwazwa na mafundisho fulani ya Yesu, andiko hilo linasema “tangu mwanzo Yesu alijua ni nani wale waliokuwa hawaamini na ni nani angemsaliti.” Ingawa neno “mwanzo” (Kigiriki, ar·kheʹ) linatumika katika 2 Petro 3:4 kurejelea mwanzo wa uumbaji, linaweza kutumiwa pia kurejelea wakati mwingine tofauti na ule wa uumbaji. (Lu 1:2; Yoh 15:27) Kwa mfano, mtume Petro alipoeleza kwamba roho takatifu iliwaangukia watu wa mataifa “kama vile ilivyoanguka pia juu yetu mwanzoni” ni wazi hakuwa akizungumzia mwanzo wake wa kuwa mwanafunzi au mtume bali alikuwa akizungumzia kipindi muhimu katika huduma yake, yaani, siku ya Pentekoste, 33 W.K. huo ukiwa ni ‘mwanzo’ wa kumiminwa kwa roho takatifu kwa ajili ya kusudi fulani hususa. (Mdo 11:15; 2:​1-4) Maelezo katika Lange’s Commentary on the Holy Scriptures (uku. 227) kuhusu Yohana 6:64 yanasema hivi: “Mwanzo . . . haumaanishi, mwanzo halisi wa kila kitu, . . . wala si mwanzo [wa Yesu] kumfahamu kila mmoja wao, . . . wala si mwanzo wa kuwakusanya wanafunzi Wake, au mwanzo wa huduma Yake ya Kimasihi, . . . ila ni mwanzo wa kutokea kwa ukosefu wa imani uliofichika [uliosababisha kujikwaa kwa baadhi ya wanafunzi].

Kwa njia hiyo hiyo, Yesu alimjua msaliti Wake tangu mwanzo.”​—Imetafsiriwa na kuhaririwa katika Kiingereza na P. Schaff, mwaka wa 1976; linganisha 1Yo 3:​8, 11, 12.

AGOSTI 29–SEPTEMBA 4

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 110-118

w87 3/15 24 ¶5

◆ 116:3​—“Kamba za mauti” ni nini?

Ilielekea kama kifo kilikuwa kimemfunga kwa imara sana mtunga zaburi kwa kamba zisizovunjika hata ikawa haiwezekani aponyoke. Kamba zenye kufungwa kwa imara sana kuzunguka mikono na miguu ya mtu zinaleta maumivu makali, au maumivu makali ya ghafula, na tafsiri ya Kigiriki Septuagint inafasili neno la Kiebrania la “kamba” kuwa “maumivu makali ya ghafula.” Kwa sababu hiyo, wakati Yesu Kristo alipokufa, yeye alikuwa katika mkamato imara wenye kupoozesha, au maumivu makali ya ghafula, ya kifo. Basi, wakati Yehova alipomfufua Yesu Yeye alikuwa “akiufungua uchungu wa mauti.”​—Matendo 2:24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki