MAISHA YA MKRISTO
Vijana—Msikawie Kuingia Kwenye “Mlango Mkubwa”
Inaweza kuwa rahisi kufikiri kwamba wakati wa ujana utaendelea milele na kwamba hatutakabili kamwe “siku zenye msiba” zinazotokana na uzee katika ulimwengu wa Shetani. (Mhu 12:1) Ikiwa wewe ni kijana, je, ni sawa kufikiri kwamba bado una wakati mwingi wa kufikia miradi ya kiroho, kama vile utumishi wa wakati wote?
‘Matukio yasiyotazamiwa’ huwapata watu wote, kutia ndani vijana. (Mhu 9:11) ‘Hujui uzima wako utakuwa namna gani kesho.’ (Yak 4:14) Kwa hiyo, usiahirishe kuanza kufuatilia miradi yako ya kiroho bila sababu ya msingi. Ingia kwenye “mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji” wakati bado una fursa ya kufanya hivyo. (1Ko 16:9) Hutajuta kamwe.
Baadhi ya miradi ya kiroho unayoweza kufikia:
Kuwahubiria watu wanaozungumza lugha ya kigeni
Utumishi wa painia
Kuhudhuria shule mbalimbali za kitheokrasi
Kutumikia katika kazi ya ujenzi
Utumishi wa Betheli
Kuwa mwangalizi wa mzunguko