Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp20 Na. 3 uku. 10
  • Endelea Kusali Ili Upate Kibali cha Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kusali Ili Upate Kibali cha Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SALI KUTOKA MOYONI NA KWA UNYENYEKEVU
  • TUMIA JINA LA MUNGU UNAPOSALI
  • SALI KWA LUGHA YAKO
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
wp20 Na. 3 uku. 10
A Middle Eastern man praying.

Mungu ambaye ni “Msikiaji wa sala,” anapenda kutusikiliza tunaposali kwake.​—ZABURI 65:2

Endelea Kusali Ili Upate Kibali cha Mungu

Mungu amewapa wanadamu zawadi ya pekee, yaani, uwezo wa kuwasiliana naye na kueleza hisia zao kupitia sala. Nabii Daudi alisali hivi: “Ee Msikiaji wa sala, watu wa kila aina watakujia.” (Zaburi 65:2) Lakini tunapaswa kusali kwa njia gani ili Mungu atusikilize na kutubariki?

SALI KUTOKA MOYONI NA KWA UNYENYEKEVU

Sala zako za kibinafsi zitakuwezesha kumwaga moyo wako mbele za Mungu, na kumweleza hisia zako za ndani. (Zaburi 62:8) Mwenyezi Mungu anapenda tusali kwa unyofu kutoka moyoni.

TUMIA JINA LA MUNGU UNAPOSALI

Ingawa Mungu ana majina mengi ya cheo kama vile Bwana au Mwenyezi Mungu, lakini ana jina moja tu la kibinafsi. “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu.” (Isaya 42:8) Jina Yehova linapatikana mara 7,000 hivi katika Maandiko Matakatifu. Manabii wengi walitumia jina la Mungu walipokuwa wakisali. Abrahamu alisema hivi: “Tafadhali Yehova, . . . niruhusu niendelee kuongea [nawe].” (Mwanzo 18:30) Sisi pia tunapaswa kutumia jina la Mungu, Yehova, tunaposali.

SALI KWA LUGHA YAKO

Mungu anaelewa mawazo na hisia zetu tunapozungumza kwa lugha yoyote ile. Neno Lake linatuhakikishia hivi: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.”​—Matendo 10:34, 35.

Hata hivyo, ili tupate baraka za Mungu, tunahitaji kufanya mambo mengine zaidi ya kusali. Katika makala zinazofuata tutachunguza mambo tunayopaswa kufanya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki