Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp20 Na. 3 uku. 13
  • Watu Wanaowasaidia Wengine Hupata Baraka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watu Wanaowasaidia Wengine Hupata Baraka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAANDIKO MATAKATIFU YANASEMA NINI?
  • KUMSAIDIA MTU MWENYE SHIDA KUNAHUSISHA NINI?
  • Kuwa “Msamaria Mwema” Kunamaanisha Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Wewe Hukubali Msaada wa Yehova?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Ni Nini Suluhisho la Chuki ya Kijamii?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Je, Wewe Ni “Tajiri Kwa Mungu”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
wp20 Na. 3 uku. 13
Mwanamume akitumia ramani kumwelekeza mgeni.

Je, unaweza kuwasaidia wengine licha ya umri wao, taifa lao, au dini yao?

Watu Wanaowasaidia Wengine Hupata Baraka

Watu wengi ulimwenguni hawana uwezo wa kupata chakula na makazi. Wengine hawana tumaini la wakati ujao. Tukijitahidi kuwasaidia watu wenye shida tutapata kibali cha Mungu na baraka zake.

MAANDIKO MATAKATIFU YANASEMA NINI?

“Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, Naye Atamlipa kwa anayotenda.”​—METHALI 19:17.

KUMSAIDIA MTU MWENYE SHIDA KUNAHUSISHA NINI?

Yesu alisimulia kuhusu mwanamume fulani ambaye alishambuliwa na wezi njiani na aliachwa hapo akiwa karibu kufa. (Luka 10:29-37) Lakini mwanamume fulani mgeni akasimama na kumtibu majeraha yake. Alimsaidia mwanamume huyo licha ya kwamba tamaduni zao zilitofautiana.

Mwanamume huyo mwenye fadhili hakumpa tu huduma ya kwanza na vitu alivyohitaji bali pia alimfariji na kumsaidia kupata kitulizo kutokana na hali aliyokabili.

Tunajifunza nini katika simulizi hili? Yesu alionyesha kwamba tunapaswa kuwasaidia watu wenye matatizo kadiri tuwezavyo. (Methali 14:31) Maandiko Matakatifu yanafundisha kwamba, hivi karibuni Mungu ataondoa umaskini na kuteseka. Huenda tukajiuliza, Mungu atatimiza mambo hayo lini na jinsi gani? Makala inayofuata itazungumzia baraka ambazo Muumba wetu mwenye upendo atatupatia wakati ujao.

“MUNGU HAKUNIACHA KAMWE”!

Limesimuliwa na mhamiaji kutoka Gambia

“Nilipofika Ulaya sikuwa na kitu chochote, yaani, sikuwa na kazi, pesa wala nyumba. Mafundisho niliyopata katika Maandiko Matakatifu yamenisaidia kuwa mbunifu, kufanya kazi kwa bidii na kuwasaidia wengine wanaohitaji msaada. Mungu hakuniacha kamwe na nimepata baraka nyingi kutoka kwake!”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki