Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
JUNI 5-11
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | YEREMIA 51-52
it-2 360 ¶2-3
Wamedi
Wakishirikiana na Waajemi walishinda Babiloni. Katika karne ya nane K.W.K., nabii Isaya alitabiri kwamba Yehova angewaleta “Wamedi juu [ya Babiloni], ambao hawaioni fedha kuwa kitu na ambao, kwa habari ya dhahabu, hawapendezwi nayo. Na pinde zao zitawavunja vipande-vipande hata vijana.” (Isa 13:17-19; 21:2) Neno “Wamedi” hapo huenda likahusisha pia Waajemi, hata wanahistoria wa Kigiriki mara nyingi walitumia neno hilo kujumuisha Wamedi na Waajemi. Kudharau kwao fedha na dhahabu kunaonyesha kwamba sababu yao kuu ya kushambulia Babiloni ilikuwa kulishinda na si kukusanya nyara, kwa hiyo hakuna rushwa wala zawadi ambayo ingewazuia kutimiza jambo walilokusudia. Kama Waajemi, Wamedi walitumia upinde kama silaha yao kuu. Inawezekana kwamba pinde zao za miti, ambazo nyakati nyingine zilipakwa shaba (linganisha Zb 18:34), ‘ziliwavunja vipande-vipande hata vijana’ wa Babiloni kwa kuwamiminia mishale mingi sana, ambayo ilikuwa imesuguliwa ili iweze kupenya ndani zaidi kwa urahisi.—Yer 51:11.
Yeremia aliandika (51:11, 28) kwamba “wafalme wa Wamedi” walikuwa kati ya wale waliovamia Babiloni. Maneno hayo ya wingi labda yanaonyesha kwamba chini ya Koreshi, huenda kulikuwa na mfalme au wafalme wengine wa Uajemi waliotawala kwa mamlaka ndogo kuliko yake, hali ambayo ilikuwa kinyume kabisa na mazoea ya kale. (Linganisha pia na Yer 25:25.) Pia tunaona kwamba Babiloni lilipotekwa na muungano wa majeshi ya Wamedi, Waajemi, Waelami, na makabila mengine jirani, ni Mmedi aliyeitwa Dario “aliyekuwa amefanywa kuwa mfalme juu ya ufalme wa Wakaldayo,” na ni wazi kwamba alichaguliwa na Mfalme Koreshi wa Uajemi.—Da 5:31; 9:1; ona DARIO Na. 1.
it-2 459 ¶4
Nabonido
Inapendeza kwamba Maandishi ya Matukio ya Nabonido yanasema hivi kuhusu usiku ambao Babiloni lilianguka: “Jeshi la Koreshi liliingia Babiloni bila kupigana.” Inaelekea inamaanisha waliingia bila vita na jambo hilo linapatana kabisa na unabii wa Yeremia kwamba ‘wanaume wenye nguvu wa Babiloni wameacha kupigana.’—Yer 51:30.
it-1 237 ¶1
Babiloni
Tangu mwaka huo muhimu, 539 K.W.K, utukufu wa Babiloni ulianza kufifia jiji hilo lilipoanguka. Wababiloni waliasi mara mbili dhidi ya maliki Mwajemi Dario I (Haistaspo), na katika kisa cha pili jiji hilo lilibomolewa. Jiji hilo liliporekebishwa kidogo liliasi tena dhidi ya Shasta wa I na likashambuliwa na kuporwa. Aleksanda Mkuu alikusudia kulifanya jiji la Babiloni kuwa mji wake mkuu, lakini alikufa ghafla mwaka wa 323 K.W.K. Niketa alishinda jiji hilo mwaka wa 312 K.W.K. na alisafirisha vitu vingi kutoka katika jiji hilo mpaka kwenye kingo za Mto Tigri kwa ajili ya kuvitumia kujenga jiji lake jipya la Seleukia. Hata hivyo, jiji hili na makazi ya Wayahudi yaliendelea kuwapo kufikia wakati wa mapema wa Ukristo, na hiyo ndiyo sababu mtume Petro alienda kutembelea jiji hilo la Babiloni, kama alivyoonyesha kwenye barua yake. (1Pe 5:13) Maandishi yaliyopatikana katika jiji hilo yanaonyesha kwamba hekalu la Babiloni la Beli lilikuwapo mpaka mwishoni mwa mwaka wa 75 W.K. Kufikia karne ya nne W.K. jiji hilo lilikuwa magofu, na mwishowe likaacha kuwepo. Mbali na “marundo ya mawe,” halina kitu kingine tena.—Yer 51:37.
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-2 444 ¶9
Milima
Inawakilisha serikali. Katika Biblia milima inaweza kuwakilisha falme au serikali zinazotawala. (Da 2:35, 44, 45; linganisha Isa 41:15; Ufu 17:9-11, 18.) Babiloni lilisababisha uharibifu wa maeneo mengine kwa kutumia mashambulizi yake ya kijeshi, na kwa hiyo, liliitwa “mlima wenye kuharibu.” (Yer 51:24, 25) Zaburi ikisimulia utendaji wa Yehova dhidi ya wanaume wa vita, inamwonyesha akiwa ‘amefunikwa na nuru, na ana utukufu kuliko milima ya mawindo.’ (Zb 76:4) “Milima ya mawindo” inaweza kuwakilisha falme zenye jeuri. (Linganisha Nah 2:11-13.) Akizungumza kumhusu Yehova, Daudi alisema hivi: “Umeusimamisha mlima wangu katika nguvu,” labda akimaanisha kwamba Yehova alikuwa ameutukuza ufalme wa Daudi na kuuimarisha. (Zb 30:7; linganisha 2Sa 5:12.) Ukweli wa kwamba milima inaweza kuwakilisha falme unamsaidia mtu kuelewa kile kinachoelezwa kwenye Ufunuo 8:8 kuwa “kitu fulani kama mlima mkubwa unaowaka moto.” Kufananishwa na mlima unaowaka moto kunaweza kudokeza kwamba ni aina ya utawala ambao unatokeza uharibifu kama moto.
it-2 882 ¶3
Bahari
Mafuriko ya wanajeshi. Yeremia alifafanua sauti ya wavamizi wa Babiloni kuwa “kama bahari ambayo imechafuka.” (Yer 50:42) Hivyo, alipotabiri kwamba “bahari” ingekuja juu ya Babiloni, kwa hakika alimaanisha mafuriko ya wanajeshi waliovamia ambayo yaliongozwa na Wamedi na Waajemi.—Yer 51:42; linganisha Da 9:26.
JUNI 19-25
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 1-5
it-1 1214
Matumbo
Chakula humeng’enywa kwenye matumbo. Jambo hilo limetumiwa kama tamathali ya usemi kuwakilisha mmeng’enyo wa kiroho au kiakili ambao katika maono, Ezekieli aliambiwa ale kitabu cha kukunjwa, na hivyo kujaza matumbo yake (Heb., me·ʽimʹ) kwa kitabu hicho. Ezekieli angepata nguvu za kiroho kwa kutafakari na kuhifadhi katika kumbukumbu yake maneno yaliyoandikwa katika kitabu hicho cha kukunjwa. Hivyo, alitiwa nguvu kiroho na kupata ujumbe wa kusema.—Eze 3:1-6; linganisha Ufu 10:8-10.