Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr17 Julai kur. 1-2
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2017
  • Vichwa vidogo
  • JULAI 10-​16
  • JULAI 31–AGOSTI 6
Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2017
mwbr17 Julai kur. 1-2

Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

JULAI 10-​16

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 15-​17

w88 9/15 17 ¶8

Yehova Achomoa Upanga Wake Kutoka Ala!

8 Ndipo, watawala wa Babuloni na Misri wakafananishwa na tai wakubwa. Mmoja alivunja sehemu ya juu ya mwerezi kwa kuondoa Mfalme Yehoyakini na kuweka Sedekia mahali pake. Ingawa Sedekia alifanya kiapo cha ushikamanifu kwa Nebukadreza, yeye alikivunja, akitafuta msaada wa kijeshi wa mtawala wa Misri, yule tai mkubwa mwingine. Ikiwa Sedekia alitaja jina la Mungu wakati wa kufanya kiapo chake, kukivunja kulileta suto juu ya Yehova. Ile fikira yenyewe tu ya kuleta suto juu ya Mungu inapasa ituzuie tusifanye kamwe ubandia kuhusiana na ahadi yetu. Sisi tumependelewa kweli kweli kuchukua jina la kimungu tukiwa Mashahidi wa Yehova!​—Ezekieli 17:​1-21.

Kutafuta Hazina za Kiroho

w88 9/15 17 ¶7

Yehova Achomoa Upanga Wake Kutoka Ala!

7 Kwa sababu ya wakaaji wayo wasio waaminifu, Yuda ilifananishwa na mzabibu-mwitu usio na tunda jema na wenye kufaa kutiwa motoni tu. (Ezekieli 15:​1-8) Ilifananishwa pia na mtoto-mwokotwa aliyeokolewa na Mungu kutoka Misri na kulelewa mpaka akafikia kuwa mwanamke mzima. Yehova alimchukua akawa mke wake, lakini yeye akageukia miungu bandia na angepatwa na uharibifu kwa ajili ya uzinzi wake wa kiroho. Hata hivyo, Mungu angeanzisha ‘agano la milele’ pamoja na walio waaminifu​—agano jipya pamoja na Israeli wa kiroho.​—Ezekieli 16:​1-63; Yeremia 31:​31-34; Wagalatia 6:16.

JULAI 31–AGOSTI 6

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 24-​27

si 133 ¶4

Kitabu cha Biblia Namba 26​—Ezekieli

4 Uthibitisho zaidi wa uasilia wapatikana katika utimizo wenye kutazamisha wa unabii mbalimbali wa Ezekieli juu ya mataifa jirani, kama vile Tiro, Misri, na Edomu. Kwa kielelezo, Ezekieli alitoa unabii wa kwamba Tiro lingefanywa ukiwa, na jambo hilo lilitimizwa kwa sehemu wakati Nebukadreza alipoteka jiji lile baada ya mazingiwa ya miaka 13. (Eze. 26:2-21) Pambano hilo halikumaanisha mwisho kamili wa Tiro. Hata hivyo, hukumu ya Yehova ilikuwa kwamba Tiro lapasa kuharibiwa kikamili. Yeye alikuwa ametabiri hivi kupitia Ezekieli: “Nitakwangua hata mavumbi yake yamtoke, na kumfanya kuwa jabali tupu. . . . Nao wataweka mawe yako, na miti yako, na mavumbi yako, kati ya maji.” (26:4, 12) Yote hayo yalitimizwa zaidi ya miaka 250 baadaye wakati Aleksanda Mkuu alipokuja juu ya jiji la kisiwani la Tiro. Askari za Aleksanda walikwangua mabomoko ya jiji la barani la Tiro lililoharibiwa na kuyatupa ndani ya bahari, wakifanyiza njia kubwa ya kupita juu ya maji ya meta 800 ya kwenda kwenye jiji la kisiwani. Halafu, kwa kutumia ufundi wa hali ya juu sana wa kimazingiwa, wakapanda zile kuta za meta 46 na kuteka jiji katika 332 K.W.K. Maelfu waliuawa, na wengi zaidi wakauzwa utumwani. Kama vile Ezekieli alivyokuwa ametabiri pia, Tiro likawa ‘jabali tupu na mahali pa kutandazia nyavu.’ (26:14) Upande ule mwingine wa Bara Lililoahidiwa, Waedomi wenye hila waliangamizwa pia, kwa utimizo wa unabii wa Ezekieli. (25:12, 13; 35:2-9) Na, bila shaka, unabii mbalimbali wa Ezekieli juu ya uharibifu wa Yerusalemu na kurejeshwa kwa Israeli ulithibitika kuwa sahihi pia.​—17:12-21; 36:7-14.

ce 216 ¶3

Je, Kweli Biblia Imeongozwa na roho ya Mungu?

3 Tiro ilikuwa bandari mashuhuri ya Foinike ambayo ilikuwa imelitendea kwa hila Israeli la kale, nchi ya waabudu wa Yehova iliyokuwa upande wa kusini. Kupitia nabii anayeitwa Ezekieli, Yehova alitabiri uharibifu kamili wa jiji hilo miaka zaidi ya 250 kabla ya uharibifu huo kutokea. Yehova alitangaza hivi: “Nitainua mataifa mengi juu yako . . . Na hakika wao wataziharibu kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nami nitakwangua mavumbi yake kutoka kwake na kumfanya kuwa uso ulio wazi na wenye kung’aa wa mwamba. Atakuwa uwanja wa kukaushia nyavu za kukokota katikati ya bahari.” Pia Ezekieli alitaja kimbele jina la taifa la kwanza na kiongozi atakayezingira Tiro: “Juu ya Tiro ninamleta Nebukadreza mfalme wa Babiloni.”​—Ezekieli 26:​3-5, 7.

it-1 70

Aleksanda

Badala ya kuwafuatilia Waajemi waliokuwa wakikimbia baada ya kushindwa mara mbili kwenye eneo la Asia Ndogo (mara ya kwanza kwenye Mto Granicus; mara ya pili kwenye eneo tambarare la Iso, ambapo jeshi kubwa la Waajemi linalokadiriwa kufikia idadi ya wanajeshi nusu milioni lilishindwa), Aleksanda aligeuzia fikira zake jiji la kisiwani la Tiro. Karne kadhaa mapema ilikuwa imetabiriwa kwamba kuta, minara, nyumba, na hata mavumbi ya Tiro yangetupwa baharini. (Eze 26:​4, 12) Kwa hiyo, lilikuwa jambo muhimu kwamba Aleksanda alitumia kifusi cha jiji la bara lililoharibiwa na Nebukadneza miaka kadhaa mapema kujenga barabara ya mita 800 juu ya bahari ili kufika kwenye jiji hilo la kisiwani. Julai 332 K.W.K., jeshi lake la wanamaji na vifaa vya vita viliponda na kuliharibu jiji hilo lenye kiburi la baharini.

Kutafuta Hazina za Kiroho

w88 9/15 21 ¶24

Yehova Achomoa Upanga Wake Kutoka Ala!

24 Ndipo, Ezekieli alipaswa kutenda kwa njia isiyo ya kikawaida. (Soma Ezekieli 24:​15-18.) Kwa nini mnabii huyo hakupaswa kuonyesha kihoro cho chote wakati mke wake alipokufa? Ili aonyeshe jinsi Wayahudi wangeshangazwa sana na uharibifu wa Yerusalemu, wakaaji wao, na lile hekalu. Tayari Ezekieli alikuwa amesema ya kutosha juu ya mambo hayo na hangenena tena ujumbe wa Mungu mpaka aletewe ripoti ya kwamba Yerusalemu ulikuwa umeanguka. Vivyo hivyo, Jumuiya ya Wakristo na wanadini wake walio wanafiki watashangazwa sana wakati wa kuharibiwa kwao. Na baada ya “dhiki kubwa” kuanza, mambo ambayo tayari jamii ya mlinzi aliyepakwa mafuta ilikuwa imekwisha kuyasema juu ya mwisho wake yatakuwa yametosha. (Mathayo 24:21) Lakini wakati “upanga” wa Mungu utakaposhuka juu ya Jumuiya ya Wakristo, wanadini hao wenye kushangazwa sana na wengine watalazimika ‘kujua ya kuwa yeye ndiye Yehova.’​—Ezekieli 24:​19-27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki