HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZEKARIA 1-8
“Shika Upindo wa Nguo ya Mtu Aliye Myahudi”
Watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa watashika kwa nguvu joho la mtu aliye Myahudi, wakisema: “Tutakwenda pamoja nanyi.” Katika siku hizi za mwisho, watu wa mataifa yote wanamiminika kumwabudu Yehova pamoja na Wakristo watiwa-mafuta
Kondoo wengine wanawategemeza watiwa-mafuta katika njia zipi?
Wanashiriki kwa moyo wote katika kazi ya kuhubiri
Wanategemeza kwa moyo wote kazi hiyo kwa kutoa michango