HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATHAYO 25
“Endeleeni Kukesha”
Ingawa Yesu alielekeza mfano wa mabikira kumi kwa wafuasi wake watiwa-mafuta, ujumbe wake muhimu unawahusu Wakristo wote. (w15 3/15 12-16) “Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamjui ile siku wala saa.” (Mt 25:13) Je, unaweza kueleza mfano wa Yesu?
Bwana harusi (mst. 1)—Yesu
Mabikira wenye busara waliojitayarisha (mst. 2)—Wakristo watiwa-mafuta ambao wamejitayarisha kutimiza mgawo wao kwa uaminifu na ambao wanaangaza daima kama mianga hadi mwisho (Flp 2:15)
Mwito: “Huyu hapa Bwana harusi!” (mst. 6)—Uthibitisho wa kuwapo kwa Yesu
Mabikira wapumbavu (mst. 8)—Wakristo watiwa-mafuta ambao wanaenda kumpokea Bwana harusi lakini hawaendelei kukesha na hawadumishi utimilifu wao
Mabikira wenye busara wanakataa kuwapa wenzao mafuta (mst. 9)—Baada ya muhuri wa mwisho, itakuwa kuchelewa sana kwa watiwa-mafuta waaminifu kuwasaidia wale walioacha kuwa waaminifu
“Bwana harusi akaja” (mst. 10)—Yesu anakuja karibu na mwisho wa dhiki kuu ili kuhukumu
Mabikira wenye busara wanaingia kwenye karamu ya ndoa pamoja na Bwana harusi, na mlango unafungwa (mst. 10)—Yesu anawakusanya watiwa-mafuta waaminifu kwenda mbinguni, lakini wasio waaminifu wanapoteza thawabu yao ya kwenda mbinguni