MAISHA YA MKRISTO
Upendo Unawatambulisha Wakristo wa Kweli—Kataa Kabisa Ubinafsi na Usiwe Mwenye Kuchokozeka
KWA NINI NI MUHIMU: Yesu alifundisha kwamba upendo ungewatambulisha wafuasi wake. (Yoh 13:34, 35) Ili tuonyeshe upendo kama wa Kristo, ni lazima tutafute faida za wengine na tusiwe wenye kuchokozeka.—1Ko 13:5.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Mtu anaposema au kufanya jambo linalokuumiza, tua na uchunguze chanzo cha tatizo na matokeo ya hatua ambayo unafikiria kuchukua.—Met 19:11
Kumbuka kwamba sisi sote si wakamilifu, na nyakati fulani tunasema au kufanya mambo ambayo tunajutia baadaye
• Tatua matatizo upesi
TAZAMENI VIDEO ‘IWENI NA UPENDO KATI YENU WENYEWE’—KATAA KABISA UBINAFSI NA USIWE MWENYE KUCHOKOZEKA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Larry aliitikiaje Tom alipotoa pendekezo?
Kutua ili kutafakari kulimsaidiaje Tom aepuke kuchokozeka?
Jibu la Tom la upole lilitulizaje hali?
Tunanufaishaje kutaniko tukiwa watulivu tunapochokozwa?