MAISHA YA MKRISTO
Yehova Alitufundisha Kuwalea Watoto Wetu
Wenzi wa ndoa wanaweza kujifunza nini kutoka kwa Baba yao wa mbinguni, Yehova, ambacho kitawasaidia kuwalea watoto wao kwa mafanikio? Tazameni video Yehova Alitufundisha Kuwalea Watoto Wetu, kisha mjibu maswali yafuatayo kuhusu Abilio na Ulla Amorim:
Malezi waliyopata yaliwatayarishaje kwa ajili ya kuwalea watoto wao?
Watoto wao wanakumbuka mambo gani mazuri waliyofurahia?
Abilio na Ulla walitumiaje andiko la Kumbukumbu la Torati 6:6, 7?
Kwa nini hawakuwalazimisha watoto wao wafuate sheria zao?
Waliwasaidiaje watoto wao kufanya maamuzi mazuri maishani mwao?
Sikuzote waliwatia moyo watoto wao wafuatilie utumishi wa wakati wote licha ya kwamba wazazi hao wangehitaji kujidhabihu kwa njia gani? (bt 178 ¶19)