HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATENDO 21-22
“Mapenzi ya Yehova na Yatendeke”
Paulo alihisi kwamba roho takatifu ilikuwa ikimwongoza aende Yerusalemu, ambako matatizo yalikuwa yakimsubiri. (Mdo 20:22, 23) Kwa hiyo, Wakristo wenye nia nzuri walipomwomba asiende, aliwajibu hivi: “Kwa nini mnalia na kujaribu kunivunja moyo?” (Mdo 21:13) Hatupaswi kuwavunja moyo wengine wanapoamua kujidhabihu kwa ajili ya utumishi wa Yehova.