HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATENDO 25-26
Paulo Akata Rufaa kwa Kaisari Kisha Amtolea Ushahidi Mfalme Herode Agripa
Ingawa hatuhitaji kuhangaikia tutakayosema “[tutakapopelekwa] mbele ya magavana na wafalme,” tunapaswa “[kuwa] tayari kujitetea” mbele ya kila mtu anayetuuliza sababu ya tumaini tulilo nalo. (Mt 10:18-20; 1Pe 3:15) Wapinzani wanapojaribu “[kutunga] matatizo kwa kutumia sheria,” tunawezaje kuiga mfano wa Paulo?—Zb 94:20.
Tunatumia maandalizi ya kisheria yanayopatikana ili kutetea habari njema.—Mdo 25:11
Tunazungumza kwa heshima na wenye mamlaka.—Mdo 26:2, 3
Ikiwezekana, tunawaeleza jinsi habari njema zimetunufaisha sisi na wengine.—Mdo 26:11-20