Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
MACHI 4-10
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAROMA 12-14
“Kuonyesha Upendo wa Kikristo Kunamaanisha Nini? ”
it-1 55
Upendo
Upendo wa kindugu (Kig., phi·la·del·phiʹa, kihalisi, “upendo kwa ndugu”) unapaswa kuwepo kati ya washiriki wote wa kutaniko la Kikristo. (Ro 12:10; Ebr 13:1; tazama pia 1Pe 3:8.) Hivyo, mahusiano katika kutaniko yanapaswa kuwa ya karibu, yenye nguvu, na yenye shauku kama ilivyo katika familia halisi. Ingawa washiriki wa kutaniko tayari wanaonyesha upendo wa kindugu, wanahimizwa kufanya hivyo kikamili zaidi.—1Th 4:9, 10.
Neno la Kigiriki phi·loʹstor·gos, linalomaanisha “kuwa na upendo mwororo,” linatumiwa kuhusu mtu aliye na uhusiano wa karibu sana na mtu mwingine. Mzizi mmoja wa fungu hilo la maneno, sterʹgo, mara nyingi unatumiwa kurejelea upendo wa asili kati ya watu wa familia moja. Mtume Paulo aliwatia moyo Wakristo wasitawishe sifa hiyo. (Ro 12:10) Pia, Paulo alionyesha kwamba siku za mwisho zingekuwa na watu “wasio na upendo wa asili” (Kig., aʹstor·goi) na kwamba watu wa aina hiyo wanastahili kifo.—2Ti 3:3; Ro 1:31, 32.
MACHI 11-17
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAROMA 15-16
Kutafuta Hazina za Kiroho
‘Mtihani wa Unyofu wa Upendo Wako’
Kwa uhakika, ndugu zao wasio Wayahudi wangalipaswa kusukumwa na moyo wawasaidie kuhusu shida yao kubwa. Ingawaje, wao walikuwa na “deni” la maalumu kwa Wakristo katika Yerusalemu. Je! si Yerusalemu ambako habari njema zilitoka zikaenea kuwafikia wasio Wayahudi? Paulo alichukua hivi: “Ikiwa Wakristo Wayahudi walishiriki hazina zao za kiroho pamoja na wasio Wayahudi, ni wazi kwamba wasio Wayahudi wana wajibu wa kuchangia mahitaji yao ya kimwili.”—Warumi 15:27, The New English Bible.
it-1 858 ¶5
Kujua Mambo Mapema, Kuamuliwa Mapema
Masihi, au Kristo angekuja kuwa Uzao ulioahidiwa ambaye kupitia yeye watu wote waadilifu kutoka katika familia zote za dunia wangebarikiwa. (Gal 3:8, 14) “Uzao” huo unatajwa kwa mara ya kwanza baada ya uasi katika Edeni, lakini kabla ya kuzaliwa kwa Abeli. (Mwa 3:15) Hilo lilitukia miaka 4,000 hivi kabla ya “siri takatifu” kufunuliwa na “uzao” kutambulishwa wazi kuwa Masihi. Hivyo, ni kweli kwamba habari hiyo “ilikuwa imefichwa tangu nyakati za zamani.”—Ro 16:25-27; Efe 1:8-10; 3:4-11.
MACHI 18-24
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 1 WAKORINTHO 1-3
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-2 1193 ¶1
Hekima
Hivyo, ulimwengu kulingana na hekima yake ulikataa uandalizi wa Mungu kupitia Kristo na kuuona kuwa upumbavu; na watawala wake, hata ikiwa walikuwa waamuzi wenye uwezo, “[walimtundika] kwenye mti Bwana mwenye utukufu.” (1Ko 1:18; 2:7, 8) Lakini Mungu, kwa upande wake, alikuwa akithibitisha kwamba hekima ya watu walio na hekima katika ulimwengu ni upumbavu. Aliwaaibisha wanaume wenye hekima kwa kutumia kile walichokiona kuwa “kitu kipumbavu cha Mungu,” na vilevile watu waliowaona kuwa “vitu vinyonge vya ulimwengu na vitu vinavyodharauliwa, vitu ambavyo si kitu,” kutimiza kusudi Lake lisiloweza kushindwa. (1Ko 1:19-28) Paulo aliwakumbusha Wakristo Wakorintho kwamba “hekima ya mfumo huu wa mambo [na] ile ya watawala wa mfumo huu wa mambo” itaangamizwa; hivyo hekima hiyo haikuwa sehemu ya ujumbe wa kiroho alioandika mtume Paulo. (1Ko 2:6, 13) Aliwaonya Wakristo jijini Kolosai dhidi ya kuvutwa na “falsafa [phi·lo·so·phiʹas, kihalisi, kupenda hekima] na udanganyifu mtupu kulingana na mapokeo ya wanadamu.”—Kol 2:8; linganisha mstari wa 20-23.
MACHI 25-31
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 1 WAKORINTHO 4-6
“Chachu Kidogo Huchachisha Donge Lote”
it-2 230
Chachu
Mtume Paulo alitumia mfano kama huo alipoliamuru kutaniko la Kikristo jijini Korintho limwondoe kutanikoni mwanamume mwenye maadili mapotovu, akisema hivi: “Je, hamjui kwamba chachu kidogo huchachisha donge lote? Ondoeni chachu ya zamani, ili muwe donge jipya, kwa kuwa ninyi hamna chachu. Kwa maana, kwa kweli, Kristo mwanakondoo wetu wa Pasaka ametolewa dhabihu.” Kisha akaonyesha waziwazi alimaanisha nini alipozungumzia “chachu”: “Basi na tufanye sherehe, si kwa chachu ya zamani, wala kwa chachu ya ubaya na uovu, bali kwa mikate isiyo na chachu ya unyoofu na kweli.” (1Ko 5:6-8) Paulo alikuwa akitumia wazo la Sherehe ya Kiyahudi ya Mikate Isiyotiwa Chachu, ambayo iliadhimishwa mara tu baada ya sherehe ya Pasaka. Kama kiasi kidogo sana cha chachu kinavyoweza kufanya donge zima la mkate liwe na chachu baada ya muda mfupi, ndivyo kutaniko hilo likiwa kikundi lingepoteza msimamo safi machoni pa Yehova ikiwa halingeondoa uvutano huo wenye kuharibu wa mtu huyo mwenye maadili mapotovu. Walipaswa kuchukua hatua kuondoa “chachu” hiyo miongoni mwao, kama tu ambavyo Waisraeli hawakuruhusu chachu nyumbani mwao wakati wa sherehe hiyo.
it-2 869-870
Shetani
Ni nini kinachomaanishwa na ‘kumkabidhi mtu wa namna hiyo kwa Shetani kwa ajili ya kuangamizwa kwa mwili’?
Alipotoa maagizo kwa kutaniko la Korintho kuhusu hatua waliyopaswa kuchukua dhidi ya mshiriki wa kutaniko aliyekuwa akifanya uovu wa kulala na mke wa baba yake, mtume Paulo aliandika hivi: “Mumkabidhi mtu wa namna hiyo kwa Shetani kwa ajili ya kuangamizwa kwa mwili.” (1Ko 5:5) Hiyo ilikuwa amri ya kumwondoa mtu huyo kutanikoni, na kumzuia asishirikiane kabisa na wengine. (1Ko 5:13) Kumkabidhi kwa Shetani kungemwondoa kutanikoni na kumwingiza katika ulimwengu ambao Shetani ndiye mungu na mtawala. Kama tu “chachu kidogo” kwenye “donge lote” la unga, mtu huyo alikuwa “mwili,” au kitu cha kimwili ndani ya kutaniko; na kwa kumwondoa mtu huyo mwenye maadili mapotovu, kutaniko hilo linalotanguliza mambo ya kiroho lingeangamiza “mwili” kutoka miongoni mwake. (1Ko 5:6, 7) Vivyo hivyo, Paulo aliwatia Himenayo na Aleksanda mkononi mwa Shetani, kwa sababu walikuwa wameiacha imani na dhamiri njema na imani yao ikavunjika.—1Ti 1:20.
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-2 211
Sheria
Sheria kwa Malaika. Malaika, ambao ni wakuu kuliko wanadamu, wako chini ya sheria na amri za Mungu. (Ebr 1:7, 14; Zb 104:4) Yehova hata alimwamuru na kumzuia adui yake Shetani. (Ayu 1:12; 2:6) Alipokuwa akibishana na Ibilisi, Mikaeli, yule malaika mkuu alitambua na kuheshimu cheo cha Yehova akiwa Mwamuzi Mkuu aliposema hivi: “Yehova na akukemee.” (Yud 9; linganisha Zek 3:2.) Yehova Mungu amempa Yesu Kristo aliyetukuzwa mamlaka juu ya malaika wote. (Ebr 1:6; 1Pe 3:22; Mt 13:41; 25:31; Flp 2:9-11) Hivyo, malaika alitumwa aende kwa Yohana, kwa amri ya Yesu. (Ufu 1:1) Hata hivyo, kwenye 1 Wakorintho 6:3 mtume Paulo alisema kwamba ndugu wa kiroho wa Kristo wamepewa daraka la kuwahukumu malaika, inaelekea kwa sababu watashiriki kwa njia fulani katika kutekeleza hukumu dhidi ya roho waovu.