Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
OKTOBA 14-20
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-2 565 ¶3
Mwangalizi
Mwangalizi Mkuu Zaidi. Ni wazi kwamba 1 Petro 2:25 inanukuu andiko la Isaya 53:6 kuhusiana na wale ambao ‘kama kondoo walipotea njia,’ kisha Petro akasema: “Lakini sasa mmerudi kwa mchungaji na mwangalizi wa nafsi zenu.” Bila shaka, maneno hayo yanamrejelea Yehova Mungu, kwa kuwa wale ambao Petro aliwaandikia hawakuwa wamepotea na kumwacha Yesu Kristo, badala yake, kupitia Yesu, walikuwa wameongozwa kurudi kwa Yehova Mungu ambaye ndiye Mchungaji Mkuu wa watu wake. (Zab 23:1; 80:1; Yer 23:3; Eze. 34:12) Yehova pia ni mwangalizi, yeye ndiye anayetuchunguza. (Zab 17:3) Uchunguzi (Kig., e·pi·sko·peʹ) anaofanya unaweza kuhusianishwa na jinsi anavyotekeleza hukumu, kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza W.K. Yerusalemu liliposhindwa kutambua wakati wake wa “kukaguliwa [Kig., e·pi·sko·pesʹ].” (Lu 19:44) Au uchunguzi huo unaweza kuleta matokeo mazuri, kama itakavyokuwa kwa wale watakaokuwa wakimtukuza Mungu katika siku “ya ukaguzi wake [Kig., e·pi·sko·pesʹ].”—1Pet 2:12.