HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 18-19
“Mwamuzi wa Dunia Yote” Aangamiza Sodoma na Gomora
Tunajifunza nini kutokana na matendo ya Yehova dhidi ya Sodoma na Gomora?
Yehova hataendelea kuvumilia uovu milele
Wale watakaookoka hukumu inayokuja ni wale wanaozingatia mapenzi ya Mungu na kuyafanya.—Lu 17:28-30
JIULIZE HIVI: ‘Je, ninataabishwa na mwenendo mpotovu wa ulimwengu huu?’ (2Pe 2:7) ‘Je, maisha yangu ya kila siku yanaonyesha kwamba kufanya mapenzi ya Mungu ndilo jambo muhimu zaidi kwangu?’