HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 40-41
Yehova Amwokoa Yosefu
Yosefu aliteseka akiwa mtumwa na mfungwa kwa miaka 13 hivi kabla ya Yehova kumwokoa. Badala ya kuwa mchungu, Yosefu alijifunza kutokana na mambo aliyokabili. (Zb 105:17-19) Alijua kwamba Yehova hakumwacha kamwe. Yosefu alifanyaje yote awezayo kulingana na hali yake?
Alikuwa mwenye bidii na mwenye kutegemeka, na hivyo kumpa Yehova msingi wa kumbariki.—Mwa 39:21, 22
Alipendezwa na wengine badala ya kupanga jinsi ya kulipiza kisasi dhidi ya wale waliomtendea vibaya.—Mwa 40:5-7
Mambo ambayo Yosefu alikabili yananisaidiaje kuvumilia matatizo yangu?
Mpaka Yehova atakaponiokoa wakati wa Har–Magedoni, ninawezaje kufanya yote niwezayo licha ya hali zangu?