Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Januari uku. 5
  • Ilinde Ndoa Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ilinde Ndoa Yako
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kufanikiwa Katika Ndoa ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ikiwa Ndoa Imo Katika Hatua ya Kuvunjika
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Baada ya Siku ya Harusi
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Kupata Furaha Katika Zawadi ya Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
mwb21 Januari uku. 5
Mume na mke wakifurahia kufua nguo pamoja.

MAISHA YA MKRISTO

Ilinde Ndoa Yako

Yehova anachukua kwa uzito nadhiri za ndoa. Amesema kwamba ni lazima wenzi wote wawili washikamane. (Mt 19:5, 6) Miongoni mwa watu wa Mungu kuna ndoa nyingi zenye furaha. Hata hivyo, hakuna ndoa kamilifu. Matatizo hutokea. Hatupaswi kamwe kusitawisha mtazamo ulioenea kwamba suluhisho la matatizo kati ya wenzi wa ndoa ni kutengana na kutalikiana. Wenzi wa ndoa Wakristo wanaweza kuilindaje ndoa yao?

Fikiria hatua tano muhimu.

  1. Linda moyo wako kwa kuepuka mambo kama vile, kuwachezea wengine kimapenzi na burudani zisizofaa, mambo ambayo yanadhoofisha ndoa.—Mt 5:28; 2Pe 2:14.

  2. Imarisha urafiki wako na Mungu na uongeze tamaa yako ya kumpendeza katika ndoa yako.—Zb 97:10.

  3. Endelea kujivika utu mpya, na ufanye mambo madogo-madogo yanayomwonyesha mwenzi wako fadhili na yanayomfurahisha.—Kol 3:8-10, 12-14.

  4. Dumisha mawasiliano yenye heshima na yenye maana.—Kol 4:6.

  5. Toa haki ya ndoa kwa wororo na upendo.—1Ko 7:3, 4; 10:24.

Wakristo wanapoheshimu ndoa wanamwonyesha heshima Mwanzilishi wa ndoa, Yehova.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA LAZIMA “TUKIMBIE KWA UVUMILIVU”—TII SHERIA ZA SHINDANO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Sehemu ya video yenye kichwa ‘Lazima ‘Tukimbie kwa Uvumilivu’—Tii Sheria za Shindano.’ Ndugu na Dada Calou wakitabasamu baada ya hotuba ya harusi yao katika Jumba la Ufalme.

    Ingawa ndoa inaweza kuanza vizuri, ni changamoto zipi zinazoweza kutokea?

  • Sehemu ya video yenye kichwa ‘Lazima ‘Tukimbie kwa Uvumilivu’—Tii Sheria za Shindano.’ Ndugu na Dada Calou wakizungumzia kwa utulivu changamoto zao. Biblia ikiwa wazi juu ya meza.

    Kanuni za Biblia zinaweza kuwasaidiaje wale wanaohisi ndoa yao haina upendo?

  • Sehemu ya video yenye kichwa ‘Lazima ‘Tukimbie kwa Uvumilivu’—Tii Sheria za Shindano.’ Ndugu Calou akimsomea mke na binti zake wawili kitabu cha ‘Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.’

    Tumia kanuni za Biblia ili ndoa yako iwe na furaha

    Yehova amewapa sheria zipi wale waliofunga ndoa?

  • Ili ndoa ifanikiwe mume na mke wanapaswa kufanya nini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki