Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb22 Septemba uku. 5
  • Ndoa—Muungano wa Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ndoa—Muungano wa Maisha
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Useja na Ndoa?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ndoa—Zawadi Kutoka kwa Mungu Mwenye Upendo
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Kutayarisha Kwa Ajili Ya Ndoa Yenye Mafanikio
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Ndoa​—Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
mwb22 Septemba uku. 5
Wenzi wa ndoa wakishirikiana katika huduma ya shambani.

MAISHA YA MKRISTO

Ndoa​—Muungano wa Maisha

Ndoa za Kikristo zenye mafanikio zinamheshimu Yehova na kuwaletea mume na mke furaha. (Mk 10:9) Ili kuwa na ndoa yenye kudumu na yenye furaha, ni lazima Wakristo watumie kanuni za Biblia wanapochagua mwenzi.

Anzisha uchumba baada ya kupita “upeo wa ujana,” kipindi ambacho hisia za ngono zinakuwa zenye nguvu na zinafanya iwe vigumu kufanya maamuzi yenye hekima. (1Ko 7:36) Tumia kwa hekima miaka yako ya useja ili kuimarisha uhusiano wako na Mungu na kusitawisha sifa za Kikristo. Ukifanya hivyo, kuna uwezekano mkubwa kwamba utachangia ndoa yenye furaha.

Kabla ya kukubali kufunga ndoa na mtu fulani, tumia muda wa kutosha kufahamu “yule mtu wa siri wa moyoni.” (1Pe 3:4) Ukianza kuwa na shaka, zungumzia hisia zako na mtu huyo. Kama tu ilivyo na uhusiano na watu wengine, inapohusu ndoa unapaswa kufikiria zaidi kile unachoweza kumpa mwenzi wako badala ya kile utakachopokea kutoka kwake. (Flp 2:3, 4) Ukitumia kanuni za Biblia kabla ya ndoa, utakuwa ukijiwekea msingi imara wa kuwa na maisha ya ndoa yenye furaha.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUJITAYARISHA KWA AJILI YA NDOA​—SEHEMU YA 3: “HESABU GHARAMA,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Uhusiano kati ya dada huyo na Shane uliendeleaje?

  • Alitambua nini uhusiano wao ulipokuwa ukiendelea?

  • Wazazi wake walimsaidiaje, naye alifanya uamuzi gani wenye hekima?

Ndugu aliye katika uhusiano na dada anaweza kufikiria maswali yafuatayo:

Ana sifa zipi za Kikristo? Anaonyeshaje kwamba anautafuta Ufalme kwanza? Je, anaonyesha kwamba anaheshimu mwongozo wa kitheokrasi? Je, anaonyesha kwamba anawajali watu wengine?

Dada aliye katika uhusiano na ndugu anaweza kufikiria maswali yafuatayo:

Ana sifa zipi za Kikristo? Je, anatanguliza ibada na majukumu yake kutanikoni mbele ya kazi, pesa, michezo, na burudani? Anawatendeaje watu wa familia yao? Je, anaonyesha kwamba anawajali watu wengine?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki