Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb24 Julai kur. 10-16
  • Agosti 5-11

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Agosti 5-11
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
mwb24 Julai kur. 10-16

AGOSTI 5-11

ZABURI 70-72

Wimbo 59 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. ‘Kiambie Kizazi Kijacho’ Kuhusu Nguvu za Mungu

(Dak. 10)

Daudi alijionea ulinzi wa Yehova alipokuwa kijana (Zb 71:5; w99 9/1 18 ¶17)

Daudi alihisi utegemezo wa Yehova alipozeeka (Zb 71:9; g04 10/8 23 ¶3)

Daudi aliwatia moyo vijana kwa kuwasimulia mambo aliyojionea (Zb 71:​17, 18; w14 1/15 23 ¶4-5)

Familia iliyoonyeshwa katika sehemu ya juma lililopita yenye kichwa “Kanuni kwa Ajili ya Jioni ya Ibada ya Familia.” Wamewaalika wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa kwenye ibada yao ya familia na wanawasikiliza kwa furaha wenzi hao wanapowaonyesha picha na kusimulia mambo yaliyoonwa.

JIULIZE, ‘Ni mtumishi gani wa muda mrefu kutanikoni ambaye ningependa kumhoji wakati wa jioni yetu ya Ibada ya Familia?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 72:8—Ahadi ya Yehova kwa Abrahamu kwenye Mwanzo 15:18 ilitimizwaje wakati wa utawala wa Mfalme Sulemani? (it-1 768)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Zb 71:​1-24 (th somo la 5)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba anapoanza kutokeza ubishi, maliza mazungumzo kwa njia inayofaa. (lmd somo la 4 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Endeleza mazungumzo ya wakati uliopita pamoja na mtu wa ukoo ambaye anasita kujifunza Biblia. (lmd somo la 8 jambo kuu la 4)

6. Kufafanua Imani Yako

(Dak. 5) Hotuba. ijwfq 49—Kichwa: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wamebadili Baadhi ya Imani Zao? (th somo la 17)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 76

7. Mapendekezo kwa Ajili ya Ibada ya Familia

(Dak. 15) Mazungumzo.

Familia iliyoonyeshwa mapema ikiwa imesimama wakizungumza na kufanya mazoezi ya wimbo wa Ufalme.
Familia hiyo ikitazama programu ya JW Broadcasting.
Binti mmoja akimjibu mama wakati wa kipindi cha mazoezi ya Ibada ya Familia.

Jioni ya Ibada ya Familia ni wakati muhimu wa watoto kujifunza “nidhamu na maagizo ya Yehova.” (Efe 6:4) Kujifunza kunahitaji jitihada, lakini kunaweza kuwa pindi yenye kufurahisha, hasa watoto wanapositawisha hamu ya kujua mengi zaidi kuhusu kweli za Biblia. (Yoh 6:27; 1Pe 2:2) Taja mambo kadhaa kwenye sanduku “Mapendekezo ya Ibada ya Familia” ili kuwasaidia wazazi wafanye jioni ya Ibada ya Familia iwe pindi ya kujifunza na yenye kufurahisha, kisha waulize wasikilizaji maswali yafuatayo:

  • Ungependa kujaribu mapendekezo gani kati ya haya?

  • Kuna jambo lingine ambalo wewe umejionea kuwa lina manufaa?

MAPENDEKEZO YA IBADA YA FAMILIA

BIBLIA:

  • Sikilizeni rekodi ya usomaji wa Biblia wa juma hilo, au msome kwa sauti kwa zamu. Kila mshiriki wa familia anaweza kusoma maneno ya mhusika tofauti wa Biblia

  • Tayarisheni maswali kwa kutegemea usomaji wa Biblia wa kila juma. Mwombe kila mshiriki wa familia achague swali moja na kulifanyia utafiti. Kisha wanaweza kusimulia mambo waliyojifunza

  • Zusha swali au utokeze hali fulani, kisha mfanye utafiti wa kanuni za Biblia zinazofaa katika kitabu Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo

  • Igizeni sehemu fulani ya simulizi la Biblia

  • Tayarisheni kadi iliyo na mstari tofauti kila juma, kwa mfano mistari iliyo kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu—Fanya Wanafunzi, kisha mjaribu kukariri mstari huo. Jikumbusheni kadi mlizokariri majuma yaliyotangulia

  • Jifunzeni sehemu ya kitabu Furahia Maisha Milele!

  • Wape washiriki wa familia mgawo wa kutoa ripoti inayotegemea mojawapo ya makala kwenye mfululizo wenye kichwa “Majibu ya Maswali ya Biblia” au “Mistari ya Biblia Yafafanuliwa,” inayopatikana chini ya tabo ya MAFUNDISHO YA BIBLIA kwenye jw.org

MIKUTANO:

  • Tayarisheni sehemu fulani ya mkutano wa kutaniko

  • Tayarisheni maelezo mtakayotoa na mfanye mazoezi. Zingatieni muda

  • Jizoezeni kuimba nyimbo za Ufalme

  • Zungumzeni na mfanye mazoezi kuhusu mambo ambayo mtamwambia mtu kabla au baada ya mkutano ufuatao

  • Ikiwa mshiriki wa familia ana mgawo wa mwanafunzi, afanye mazoezi mbele ya familia yote

HUDUMA:

  • Jitayarisheni kwa ajili ya huduma ya nyumba kwa nyumba

  • Jitayarisheni kwa ajili ya ziara zenu za kurudia

  • Wazieni kikao kisicho rasmi, kisha fanyeni mazoezi ya kuanzisha mazungumzo ya kirafiki

  • Zungumzieni miradi hususa ya kupanua huduma yenu wakati wa majira ya Ukumbusho au wakati wa likizo ya kazi au ya shule

MAHITAJI YA FAMILIA:

  • Pangeni kipindi cha mazoezi cha jinsi ya kushughulikia hali fulani hususa ambayo imetokea au ambayo inaweza kutokea, kama zinazohusu kutounga mkono upande wowote, kuonewa, kuanzisha urafiki wa kimapenzi, au kusherehekea sikukuu

  • Pangeni kipindi cha mazoezi ambapo wazazi wanaigiza kwamba wao ni watoto na watoto wanaigiza kwamba wamechukua jukumu la wazazi. Watoto wafanye utafiti kuhusu habari fulani kisha waijadili na wazazi wao

MAPENDEKEZO YA ZIADA:

  • Tazameni programu ya JW Broadcasting® kisha mzungumze kuihusu

  • Someni makala kwenye jw.org au mtazame video, kisha mzungumze kuihusu

  • Zungumzieni jambo fulani kutoka kwenye sehemu ya “Matineja” au ya “Watoto” kwenye tabo ya MAFUNDISHO YA BIBLIA kwenye jw.org

  • Pitieni mambo makuu mliyoandika kwenye kusanyiko la eneo au la mzunguko

  • Chunguzeni au mfanye utafiti kuhusu uumbaji fulani, kisha mzungumzie unawafundisha nini kumhusu Yehova

  • Pindi kwa pindi mkaribisheni mtu kwenye ibada yenu, kisha mwombeni awaeleze alipataje kweli na amekabili changamoto zipi

  • Jiwekeeni miradi ya kiroho, na mzungumzie jinsi ya kuifikia

  • Shughulikieni mradi fulani pamoja, kama vile kujenga kitu kinachotajwa katika Biblia, kwa mfano, safina ya Noa. Au mchunguze ramani na chati kwenye Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na katika machapisho yetu

Onyesha VIDEO Endelea Kuboresha Ibada ya Familia. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Mume anawezaje kufanya mke wake afurahie ibada ya familia ikiwa hakuna watoto nyumbani?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 13 ¶17-24

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 123 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki