Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb24 Novemba kur. 4-5
  • Novemba 18-24

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Novemba 18-24
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
mwb24 Novemba kur. 4-5

NOVEMBA 18-24

ZABURI 107-108

Wimbo 7 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. “Mshukuruni Yehova, kwa Maana Yeye Ni Mwema”

(Dak. 10)

Kama tu Yehova alivyowakomboa Waisraeli kutoka Babiloni, Yehova ametuokoa kutoka katika ulimwengu wa Shetani (Zb 107:​1, 2; Kol 1:​13, 14)

Kumshukuru Yehova kunatuchochea tumsifu katika kutaniko (Zb 107:​31, 32; w07 4/15 20 ¶2)

Tunasitawisha uthamini kwa kuchunguza kwa makini matendo ya Yehova yenye upendo (Zb 107:43; w15 1/15 9 ¶4)

Picha: Njia ambazo tunaweza kumsifu Yehova. 1. Ndugu na dada wakiimba kwenye mkutano wa kutaniko. 2. Ndugu akitoa maelezo kwenye mkutano. 3. Dada wawili wakishiriki huduma ya nyumba kwa nyumba.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 108:9—Huenda ni kwa nini Moabu lililinganishwa na ‘beseni la kuogea’ la Mungu? (it-2 420 ¶4)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Zb 107:​1-28 (th somo la 5)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. (lmd somo la 1 jambo kuu la 4)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mweleze mwenye nyumba kuhusu programu yetu ya kujifunza Biblia, na umpe kadi ya mawasiliano ya masomo ya Biblia. (lmd somo la 9 jambo kuu la 3)

6. Hotuba

(Dak. 5) ijwyp 90—Kichwa: Nitaepukaje Maoni Yasiyofaa? (th somo la 14)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 46

7. Tunaimba Ili Kumshukuru Yehova

(Dak. 15) Mazungumzo.

Waisraeli walikuwa na hofu nyingi walipokabiliwa na jeshi lenye nguvu la Wamisri kwenye Bahari Nyekundu. Lakini mara tu Yehova alipowaokoa, watu hao wenye shukrani waliimba kwa shangwe. (Kut 15:​1-19) Wanaume ndio walioongoza katika kuimba wimbo huo mpya. (Kut 15:21) Yesu na Wakristo wa mapema pia walimwimbia Mungu sifa. (Mt 26:30; Kol 3:16) Leo pia tunaendelea kuonyesha uthamini wetu kwa Yehova kwa kuimba kwenye mikutano ya kutaniko na kwenye makusanyiko ya mzunguko na ya eneo. Kwa mfano, wimbo ambao tumetoka kuimba, “Asante, Yehova,” umeimbwa katika mikutano yetu tangu mwaka wa 1966.

Katika maeneo fulani, huenda wanaume wakaaibika kuimba mbele ya watu. Huenda wengine wasitake kwa sababu wanafikiri hawana sauti nzuri. Hata hivyo, tunapaswa kukumbuka kwamba kuimba kwenye mikutano yetu ni sehemu ya ibada. Tengenezo la Yehova linafanya kazi nyingi sana kutunga nyimbo zenye maneno matamu na kuchagua nyimbo zinazofaa kwa ajili ya kila mkutano. Kazi yetu ni rahisi—tunahitaji tu kuimba pamoja kwa sauti ili kuonyesha upendo na uthamini wetu kwa Baba yetu wa mbinguni.

Onyesha VIDEO Historia Yetu Hatua kwa Hatua—Zawadi ya Nyimbo, Sehemu ya 2. Kisha waulize wasikilizaji:

    Picha kutoka kwenye video “Historia Yetu Hatua kwa Hatua​—⁠Zawadi ya Nyimbo, Sehemu ya 2.” Ndugu F. W. Franz akitangaza kutolewa kwa kitabu “Kingdom Service Song Book.”
  • Ni tukio gani la pekee lililotokea mwaka wa 1944?

  • Picha kutoka kwenye video “Historia Yetu Hatua kwa Hatua​—⁠Zawadi ya Nyimbo, Sehemu ya 2.” Usiku sana, ndugu nchini Siberia akificha rekodi ya wimbo uliombwa na ndugu na dada.
  • Ndugu zetu huko Siberia walionyeshaje uthamini kwa kuimba nyimbo za Ufalme?

  • Picha kutoka kwenye video “Historia Yetu Hatua kwa Hatua​—⁠Zawadi ya Nyimbo, Sehemu ya 2.” Ndugu na dada wakiimba kwenye kusanyiko, wakiongozwa na okestra.
  • Kwa nini kuimba ni jambo muhimu sana kwa Mashahidi wa Yehova?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 18 ¶6-15

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 73 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki