NOVEMBA 25–DESEMBA 1
ZABURI 109-112
Wimbo 14 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Muunge Mkono Yesu, Mfalme!
(Dak. 10)
Yesu alipopanda kwenda mbinguni, aliketi kwenye mkono wa kuume wa Yehova (Zb 110:1; w06 9/1 13 ¶6)
Mwaka wa 1914, Yesu alianza kuwatiisha maadui wake (Zb 110:2; w00 4/1 18 ¶3)
Tunaweza kujitoa kwa hiari ili kuunga mkono utawala wa Yesu (Zb 110:3; be 76 ¶2)
JIULIZE, ‘Ninaweza kujiwekea miradi gani ili kuonyesha kwamba ninaunga mkono Ufalme?’
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Zb 110:4—Fafanua agano linalotajwa katika mstari huu. (it-1 524 ¶2)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Zb 109:1-26 (th somo la 2)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 2) NYUMBA KWA NYUMBA. Tumia trakti kuanzisha mazungumzo. (lmd somo la 4 jambo kuu la 3)
5. Kufafanua Imani Yako
(Dak. 5) Onyesho. ijwfq 23—Kichwa: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawaendi Vitani? (lmd somo la 4 jambo kuu la 4)
6. Kufanya Wanafunzi
Wimbo 72
7. Tunawezaje Kuunga Mkono Ufalme kwa Ushikamanifu?
(Dak. 15) Mazungumzo.
Njia moja ambayo Yehova ameonyesha kwamba yeye ndiye mwenye enzi kuu ya ulimwengu wote ni kwa kusimamisha Ufalme wake. (Da 2:44, 45) Hivyo, tunapounga mkono Ufalme wa Mungu, tunatetea enzi kuu ya Yehova.
Onyesha VIDEO Muunge Mkono kwa Ushikamanifu “Mkuu wa Amani.” Kisha waulize wasikilizaji:
Tunaonyeshaje kwamba tunaunga mkono kwa ushikamanifu Ufalme wa Mungu?
Andika mstari wa Biblia unaopatana na njia zifuatazo za kuunga mkono Ufalme wa Mungu.
Tunapaswa kufanya Ufalme kuwa jambo muhimu zaidi maishani mwetu.
Tunapaswa kuishi kupatana na viwango vya maadili kwa ajili ya raia wa Ufalme.
Tunapaswa kuwaeleza wengine kuhusu Ufalme kwa bidii.
Tunapaswa kuheshimu serikali za wanadamu, lakini tumtii Mungu sheria ya Kaisari inapopingana na sheria ya Mungu.
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) bt sura ya 18 ¶16-24