Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb24 Novemba kur. 12-13
  • Desemba 23-29

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Desemba 23-29
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
mwb24 Novemba kur. 12-13

DESEMBA 23-29

ZABURI 119:​121-176

Wimbo 31 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Jinsi ya Kuepuka Matatizo ya Kujisababishia

(Dak. 10)

Penda amri za Mungu (Zb 119:127; w18.06 17 ¶5-6)

Chukia kutenda mabaya (Zb 119:128; w93 4/15 17 ¶12)

Msikilize Yehova, na uepuke makosa ya ‘wasio na uzoefu’ (Zb 119:​130, 133; Met 22:3)

Biblia iliyofunguliwa ikiwa kando ya sarafu na vipande vya dhahabu.

JIULIZE, ‘Ninahitaji kufanya mabadiliko gani ili nipende amri za Mungu zaidi au nichukie mabaya?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 119:106—Kupatana na mstari huu, tunapaswa kusadiki jambo gani? (w23.01 2 ¶2)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Zb 119:​121-152 (th somo la 2)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. (lmd somo la 1 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwonyeshe mwenye nyumba jinsi ya kupata habari inayompendeza kwenye jw.org. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) Mazungumzo pamoja na mwanafunzi wa Biblia ambaye hahudhurii mikutano ya kutaniko kwa ukawaida. (lmd somo la 12 jambo kuu la 4)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 121

7. Usiruhusu Pesa Zikusababishie Maumivu Yasiyo ya Lazima

(Dak. 15) Mazungumzo.

Wale ambao maisha yao yanaongozwa na upendo wa pesa ‘wamejichoma kila mahali kwa maumivu mengi.’ (1Ti 6:​9, 10) Hapa chini kuna baadhi ya maumivu yasiyo ya lazima ambayo tunaweza kupata ikiwa tunapenda pesa na ikiwa tunaruhusu upendo huo uongoze maisha yetu.

  • Hatutaweza kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova.—Mt 6:24

  • Hatutawahi kutosheka.—Mhu 5:10

  • Itakuwa rahisi zaidi kushawishika kutenda mabaya, kama vile, kusema uwongo, kuiba, na kutenda kwa hila. (Met 28:20) Tukifanya makosa tutapatwa na hisia za hatia, sifa mbaya, na tutapoteza kibali cha Mungu

Picha kutoka kwenye video “Jinsi ya Kutumia Pesa Zako kwa Hekima.” Mvulana akiwa ameshika kibobo.

Soma Waebrania 13:​5, na kisha mzungumzie swali hili:

  • Ili tuepuke kupatwa na maumivu ya kihisia, tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu pesa, na kwa nini?

Hata ikiwa hatupendi pesa, tutapatwa na matatizo ikiwa hatuzitumii kwa hekima.

Onyesha video ya VIBONZO KWENYE UBAO Jinsi ya Kutumia Pesa Zako kwa Hekima. Kisha waulize wasikilizaji:

    Picha kutoka kwenye video “Jinsi ya Kutumia Pesa Zako kwa Hekima.” Mvulana na msichana wakiandika orodha ya mambo wanayohitaji na wanayotaka, kisha wanaandika bei ya kila bidhaa. Orodha ya mvulana inatia ndani headphones, viatu, chakula, na tiketi za treni. Orodha ya msichana huyo inatia ndani kipochi, saa, chakula, na petroli.
  • Kwa nini tunapaswa kupanga bajeti, na tunaweza kuipangaje?

  • Picha kutoka kwenye video “Jinsi ya Kutumia Pesa Zako kwa Hekima.” Msichana yule ananunua miavuli miwili huku mvua ikinyesha. Mwavuli mmoja ni wake na ule mwingine ni wa ndugu yake ambaye alitumia pesa zake kununua aiskrimu.
  • Kwa nini ni vizuri kuweka akiba fulani ya pesa?

  • Picha kutoka kwenye video “Jinsi ya Kutumia Pesa Zako kwa Hekima.” Yule mvulana amefungwa pingu kwenye kadi kubwa sana ya benki huku kadi nyingine ikitabasamu.
  • Kwa nini ni jambo la hekima kuepuka madeni yasiyo ya lazima?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 20 ¶1-7, na utangulizi wa sehemu ya 7

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 101 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki