AGOSTI 18-24
METHALI 27
Wimbo 102 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Jinsi Tunavyonufaika kwa Kuwa na Marafiki wa Kweli
(Dak. 10)
Kwa ujasiri marafiki wa kweli watatupatia shauri tunalohitaji (Met 27:5, 6; w19.09 5 ¶12)
Marafiki wa kweli wanaweza kutusaidia kwa njia bora zaidi kuliko watu wa ukoo (Met 27:10; it-2 491 ¶3)
Marafiki wa kweli wanatusaidia kuwa watu bora (Met 27:17; w23.09 10 ¶7)
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Met 27:21—Matendo yetu yanafunuaje utu wetu tunaposifiwa? (w06 9/15 19 ¶12)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Met 27:1-17 (th somo la 5)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba ni wa dini isiyo ya Kikristo. (lmd somo la 6 jambo kuu la 5)
5. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Tumia video kutoka kwenye Sanduku la Vifaa vya Kufundishia. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)
6. Hotuba
(Dak. 5) ijwyp makala ya 75—Kichwa: Nifanye Nini Rafiki Yangu Akiniumiza? (th somo la 14)
Wimbo 109
7. “Ndugu Ambaye Amezaliwa Kwa Ajili ya Nyakati za Taabu”
(Dak. 15) Mazungumzo.
Yehova ametupatia undugu wa ulimwenguni pote ambako tunaweza kupata marafiki wenye upendo. Ingawa tunaweza kuwa na urafiki na watu wengi kutanikoni, ni wangapi ambao ni marafiki zetu wa karibu? Tunakuwa na urafiki wa karibu na wengine tunapofahamiana nao vizuri, tunapotumainiana, tunapokuwa na mazungumzo ya kutoka moyoni, tunapofanya mambo pamoja na kusaidiana. Kwa hiyo, kusitawisha na kudumisha urafiki kunachukua muda na jitihada.
Soma Methali 17:17. Kisha waulize wasikilizaji:
Kwa nini ni jambo lenye hekima kusitawisha urafiki wa karibu na wengine sasa kabla ya dhiki kuu kuanza?
Soma 2 Wakorintho 6:12, 13. Kisha waulize wasikilizaji:
Kutumia mistari hii kunawezaje kutusaidia kupata marafiki?
Onyesha VIDEO “Kuna Wakati Uliowekwa wa Kila Jambo”—Kusitawisha Urafiki Kunahitaji Muda. Kisha waulize wasikilizaji:
Umejifunza nini kuhusu urafiki katika video hii?
Unaweza kupanda mbegu ya urafiki kwa kutabasamu au kwa salamu changamfu, na kuitia maji kwa kuonyesha upendezi wa kibinafsi. Uwe mwenye subira na uruhusu urafiki wenu ukue kwa kutumia wakati pamoja. Kwa kufanya hivyo, urafiki wenu utaimarika na kudumu milele.
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 10-11