AGOSTI 11-17
METHALI 26
Wimbo 88 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Kaa Mbali na Mtu “Mpumbavu”
(Dak. 10)
Mtu “mpumbavu” hastahili heshima (Met 26:1; it-2 729 ¶6)
Mara nyingi “watu wapumbavu” huhitaji nidhamu kali (Met 26:3; w87 10/1 19 ¶12)
Mtu “mpumbavu” hategemeki (Met 26:6; it-2 191 ¶4)
MAANA: Katika Biblia, neno “mpumbavu” linamfafanua mtu ambaye hakubali sababu na anatenda kwa njia inayopingana na viwango vya Mungu vya mema na mabaya.
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Met 26:4, 5—Kwa nini tunaweza kusema kwamba methali hizi mbili hazipingani? (it-1 846)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Met 26:1-20 (th somo la 5)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Tumia trakti kuanzisha mazungumzo. (lmd somo la 1 jambo kuu la 5)
5. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Endeleza mazungumzo kwa kutumia trakti ambayo ulimwachia mwenye nyumba katika ziara iliyopita. (lmd somo la 7 jambo kuu la 4)
6. Kufanya Wanafunzi
(Dak. 5) Msaidie mwanafunzi wako ajitayarishe kumtolea ushahidi mtu wake wa ukoo. (lmd somo la 11 jambo kuu la 5)
Wimbo 94
7. “Uwe Mwenye Hekima ili Upate Wokovu” Kupitia Funzo la kibinafsi
(Dak. 15) Mazungumzo.
Mtume Paulo alimkumbusha Timotheo kuhusu thamani ya maandishi matakatifu aliyojifunza tangu utoto mchanga. Maandishi hayo yalimsaidia Timotheo ‘awe mwenye hekima ili apate wokovu.’ (2Ti 3:15) Ni muhimu kwa kila Mkristo kutenga muda kwa ajili ya kusoma na kujifunza Biblia, kwa sababu kweli za Biblia ni zenye thamani sana. Lakini vipi ikiwa hatufurahii kujifunza?
Soma 1 Petro 2:2. Kisha waulize wasikilizaji:
Je, tunaweza kujifunza kufurahia kusoma Biblia?
Tunaweza kufanya nini ili ‘tukuze hamu’ ya kusoma Neno la Mungu?—w18.03 29 ¶6
Vifaa vya kielektroni vinavyotolewa na tengenezo vinawezaje kutusaidia kujifunza zaidi tunaposoma Biblia?
Onyesha VIDEO Mambo Yaliyotimizwa na Tengenezo—Mapendekezo ya Kutumia JW Library. Kisha waulize wasikilizaji:
Umenufaikaje kwa kutumia JW Library®?
Umefurahia zaidi kutumia mambo gani katika tovuti hiyo?
Ni mambo gani ambayo ungependa kujifunza katika tovuti hiyo na kuanza kuyatumia?
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 8-9