Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w20 Septemba uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Maoni Ambayo Wakristo Wanapaswa Kuwa Nayo Juu ya Ukombozi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Serikali
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Maoni ya Mkristo Kuhusu Mamlaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
w20 Septemba uku. 31
Mchoro ukimwonyesha Yehova akiwa ameketi kwenye kiti cha ufalme cha zumaridi. Mimweko ya mwangaza inazunguka kiti cha ufalme.

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, andiko la Mhubiri 5:8 linarejelea tu watawala wa kibinadamu, au linamhusu pia Yehova?

Mstari huo unaochochea fikira unasema: “Ukiona maskini wakikandamizwa kwa njia yoyote ile na haki na uadilifu zikikiukwa katika wilaya yenu, usishangazwe na jambo hilo. Kwa maana ofisa huyo mkuu anatazamwa na yule aliye juu zaidi yake, na kuna wengine walio juu zaidi yao.”​—Mhu. 5:8.

Kwa mtazamo wa kibinadamu, andiko hilo linafafanua vizuri wale wenye mamlaka katika serikali. Lakini zaidi ya hilo, mstari huo unafunua kweli fulani kumhusu Yehova, ambayo inapaswa kutufariji na kutuimarisha imani.

Andiko la Mhubiri 5:8 linarejelea mtawala ambaye anawakandamiza maskini na kuwanyima haki zao. Mtawala huyo kukumbuka kwamba anatazamwa na mtu mwingine aliye juu zaidi yake au aliye na mamlaka kubwa zaidi kuliko yeye katika serikali. Isitoshe, huenda kuna wengine walio katika cheo cha juu hata zaidi ya hao. Inasikitisha kwamba katika serikali za kibinadamu, huenda watawala hao wote ni wafisadi na ni lazima watu wa kawaida wakabiliane na hali ya kwa haki na viongozi hao wenye vyeo mbalimbali.

Hata hivyo, haidhuru hali zinavunja moyo kadiri gani, tunaweza kufarijika kwa kujua kwamba Yehova ‘anawatazama hata maofisa hao wakuu’ katika serikali za wanadamu. Tunaweza kumwomba Mungu atusaidie na tunaweza kumtupia mizigo yetu. (Zab. 55:22; Flp. 4:6, 7) Tunajua kwamba “macho ya Yehova yanaenda huku na huku duniani kote ili adhihirishe nguvu zake kwa niaba ya wale ambao moyo wao ni kamili kumwelekea yeye.”—2 Nya. 16:9.

Hivyo, Mhubiri 5:8 inatukumbusha hali halisi kuhusu viongozi katika serikali; sikuzote kuna aliye na mamlaka kubwa zaidi kuliko mwingine. Jambo la muhimu hata zaidi, mstari huo unaweza kutusaidia kukumbuka kwamba Yehova ndiye aliye juu zaidi, naam, mwenye Mamlaka Kuu Zaidi. Sasa anatawala kupitia Yesu Kristo, Mwana wake, Mfalme wa Ufalme. Mweza-Yote anayeona mambo yote, ndiye mwenye haki kamili na hana upendeleo, na ndivyo Mwana wake alivyo pia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki