Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 7/1 kur. 5-7
  • Maoni Ambayo Wakristo Wanapaswa Kuwa Nayo Juu ya Ukombozi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maoni Ambayo Wakristo Wanapaswa Kuwa Nayo Juu ya Ukombozi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kukombolewa Kwenye Mamlaka Kamili
  • Kukombolewa Kwenye Mamlaka ya Kiasi
  • “Kukombolewa” Kwenye Mamlaka Ndani ya Kundi
  • Heshima kwa Mamlaka—Kwa Nini Ni Muhimu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Maoni ya Mkristo Kuhusu Mamlaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Ukombozi—Unatamanika Kama Nini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kwa Nini Tuheshimu Mamlaka?
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 7/1 kur. 5-7

Maoni Ambayo Wakristo Wanapaswa Kuwa Nayo Juu ya Ukombozi

WAKRISTO wanapinga “Ukombozi” unaokataa mamlaka inayotumiwa kwa njia inayofaa. Kwa sababu gani? Ni kwa sababu kwa kweli hali hiyo haikomboi​—inatumikisha. Mfano mwepesi unaweza kutumiwa kuonyesha jambo hilo.

Kijana anaudhika-udhika akiwa chini ya mamlaka ya wazazi, wanaomkataza asivute sigareti na asinywe vileo. Kwa kutokuthamini kwamba wanatumia mamlaka yao kwa faida yake mwenyewe, yeye anatamani sana kukombolewa. Baada ya kuwa na umri wa kutosha na kuondoka nyumbani, mwishowe anakuwa amepata hali ya kukombolewa ambayo sikuzote alitaka. Lakini miaka mingi baadaye, baada ya kuwa mvutaji sigareti asiyeacha na kukaribia kuwa mzoelevu wa kutumia vileo, daktari wake anamwambia kwamba kwa sababu za kiafya ni lazima aache kuvuta sigareti na pia kunywa vileo. Anaona ni vigumu kufanya hivyo. Kukombolewa kwake kumemwongoza kwenye uzoelevu wa vitu hivyo, kwenye utumwa.

Kukombolewa Kwenye Mamlaka Kamili

Mamlaka ya Mungu ni kamili na yanategemea kuwa kwake Muumba. Jambo hilo linampa yeye haki ya kuamulia viumbe vyake mwenendo unaofaa, ulio wa adili na usio wa adili. Viwango hivyo, vilianzishwa kwa ajili ya masilahi ya wanadamu, vimeonyeshwa waziwazi katika Biblia. “Msidanganyike,” hiyo inasema. “Waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi.”​—1 Wakorintho 6:9, 10.

Hasa katika karne hii ya 20 yenye mambo ya hali ya juu, iliyo na hekima ya kilimwengu mwanadamu amejaribu kujikomboa mwenyewe kwenye miongozo hiyo ya adili. Hata hivyo ijapokuwa amepata kile kinachoitwa ukombozi ati, yeye hawezi kujiweka huru kutokana na matokeo ya kuzoea mambo ambayo Mungu anasema ni dhambi. Badala ya kuwa huru watu kama hao wamekuwa watumwa wa tamaa zao wenyewe, uchu na nyege, kama vile Yesu alivyoonyesha wazi aliposema hivi: “Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.”—Yohana 8:34; ona pia Warumi 6:16.

Kukombolewa Kwenye Mamlaka ya Kiasi

Maafisa wa serikali wana haki ya kutumia mamlaka ndani ya nchi, wazazi ndani ya jamaa, walimu ndani ya mfumo wa shule, na wazee Wakristo ndani ya kundi. Bila shaka, mamlaka hiyo ni ya kiasi tu. Kwa mfano, ile mamlaka kamili ya Yehova, anayeamuru kwamba watumishi wake wasome Neno lake na kushirikiana na Wakristo wenzao, ingepasa kutangulizwa mbele ya ile mamlaka ya kiasi ya mume anayeweza kudai kwamba mke wake asifanye lo lote la mambo hayo.​—Matendo 5:29.

Lakini, Wakristo wakiitambua ile mamlaka ya kiasi ya serikali, hawangeweza kushiriki katika vyama vya ukombozi ili waipindue mamlaka hiyo. Wao hawangeweza kukubaliana katika mawazo yao na maasi ya kiraia kwa sababu tu hawakubaliani na uongozi wa kiserikali, wala wao hawangeweza kutia watu moyo wasilipe kodi ili kwa njia hiyo wapinge miongozo fulani. “Amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu,” akasema mtume Paulo, akiongezea: “Nao washindanao watajipatia hukumu.”​—Warumi 13:1-4.

Lakini namna gani ikiwa afisa wa serikali anatenda udhalimu na kutumia vibaya mamlaka yake? Namna gani kama yeye anabagua watu fulani au vikundi vya wachache wasiopendwa na watu wengi? Shauri la Biblia ni: “Ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu na haki kuondolewa kwa jeuri katika jimbo, usilistaajabie hilo; kwa sababu, aliye juu kuliko walio juu huangalia.” (Mhubiri 5:8) Huenda ikawezekana kuomba rufani kwa mkuu mwenye cheo cha juu zaidi katika serikali au mahakamani. Lakini hata kama haki haitapatikani kwa njia hiyo, watumishi wa Mungu wanaweza kuwa na uhakika kwamba, “macho ya [Yehova] hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake.”​—2 Mambo ya Nyakati 16:9.

Ni hali moja kuhusiana na jamaa. Waume au akina baba wakitumia vibaya mamlaka yao, tunaweza kuwa na uhakika kwamba hatimaye Mungu atanyosha mambo hayo, kwa sababu hataruhusu udhalimu wo wote uwe katika mfumo wake mpya wenye uadilifu utakaokuja karibuni. Kwa sasa, wanawake na watoto Wakristo wanaendelea kuiheshimu kanuni ya ukichwa wa Kikristo, hata ikiwa nyakati nyingine inatumiwa vibaya. Wao wanathamini kwamba kanuni hiyo haikusudiwi ilete madhara bali ihakikishe kwamba amani na umoja vimo ndani ya jamaa na pia katika kundi la Kikristo.​—1 Wakorintho 11:3.

“Kukombolewa” Kwenye Mamlaka Ndani ya Kundi

Kwa habari ya ukichwa katika kundi la Kikristo, Neno la Mungu linasema hivi: “Iweni wenye kutii wale wanaoongoza kati yenu na kuwa wenye kunyenyekea, maana wanaendelea kulinda nafsi zenu kama wale watakaotoa sababu.” (Waebrania 13:17, NW) Ingawa mamlaka hiyo ya wazee ni ya kiasi, Mungu ameikabidhi kwao kupitia roho takatifu yake. Hivyo wao wamepewa mamlaka hiyo kwa njia iliyo ya moja kwa moja zaidi ya ile mamlaka ya kiasi iliyokabidhiwa, kwa mfano, kwa maafisa wa serikali.​—Matendo 20:28.

Watu fulani wamekuwa na maoni kwamba mielekezo na maagizo yanayotolewa na tengenezo la Mungu linaloonekana ni yenye vizuizi vingi mno, bila kuruhusu mtu awe na uhuru wake mwenyewe unaotosha. Jambo hilo limewafanya waache kushirikiana na Mashahidi wa Yehova; wakawa hawana tena nia ya kujitiisha chini ya wale wanaowalinda nafsi zao. Ingawa watu hao labda wanajifikiria au hata kujiita kuwa wamekombolewa, kwa kweli, “ukombozi” wao kwa mara nyingine kumewafanya watumwa wa imani na mazoea ya dini ya uwongo.

Wakristo wa kweli wanaheshimu mamlaka, ile mamlaka kamili ya Mungu na pia ile mamlaka ya kiasi ya wanadamu. Maoni hayo yanayofaa juu ya mamlaka yanawazuia wasitumie vibaya uhuru wa Kikristo ambao maarifa ya kuujua ukweli yamewapa.

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Mamlaka ya Mungu ni kamili na inategemea kuwa kwake Muumba

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Wakristo hawaiasi serikali kwa sababu ya miongozo itakayoifanya ipaswe kumtolea Mungu jibu

[Blabu katika ukurasa wa 7]

Wakristo wa kweli wanaheshimu mamlaka, ile mamlaka kamili ya Mungu na ile mamlaka ya kiasi ya wanadamu

[Picha katika ukurasa wa 7]

Kuilipa mamlaka ya kilimwengu haki yayo

Kutambua mamlaka ya kiasi katika kundi

Kuthamini Mamlaka Iliyo Kuu Zaidi, Yehova Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki