Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp21 Na. 1 kur. 14-15
  • Sala Zinaweza Kukusaidiaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sala Zinaweza Kukusaidiaje?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Sala​—Ina Umuhimu Gani Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
wp21 Na. 1 kur. 14-15

Sala Zinaweza Kukusaidiaje?

Pamela aliyekuwa na ugonjwa wa kansa alitafuta matibabu. Hata hivyo, alisali pia kwa Mungu ili ampe nguvu za kuvumilia ugonjwa huo. Je, kusali kwa Mungu kulimsaidia?

Pamela anasema: “Nilipokuwa nikipata matibabu ya kansa, mara nyingi niliogopa sana. Lakini niliposali kwa Yehova Mungu, nilihisi utulivu na nikaanza kufikiria mambo kwa njia nzuri. Bado ninapata maumivu makali sana lakini sala inanisaidia kudumisha mtazamo unaofaa. Watu wanaponiuliza ninahisije, ninawaambia, ‘Bado nina maumivu, lakini nina furaha!’”

Bila shaka, hatuhitaji kusubiri hadi tuwe na tatizo kubwa la afya au matatizo mengine ili tusali. Sisi sote tunakabili changamoto, kubwa na ndogo, na mara nyingi tunahisi tunahitaji msaada ili kukabiliana nazo. Je, sala zinaweza kutusaidia?

Biblia inasema: “Mtupie Yehova mzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu kamwe mwadilifu aanguke.” (Zaburi 55:22) Maneno hayo yanafariji sana. Hivyo, sala zinaweza kukusaidia kwa njia gani? Unaposali kwa Mungu kwa njia inayofaa, atakupatia kile unachohitaji ili ukabiliane na changamoto ulizo nazo.​—Ona sanduku “Unaweza Kunufaikaje kwa Kusali?”

Unaweza Kunufaikaje Kwa Kusali?

Amani ya akili

Mfanyabiashara ambaye mwanzoni alipoteza kazi, akitabasamu na kutembea kwa uhakika.

“Mjulisheni Mungu maombi yenu; na amani ya Mungu inayozidi uelewaji wote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.” (Wafilipi 4:6, 7) Ukimweleza Mungu mahangaiko yako, atakusaidia kuwa na utulivu na kutenda kwa busara hata unapokuwa na mkazo.

Hekima kutoka kwa Mungu

Mwanamke ambaye mwanzoni alikuwa akisoma sala, sasa anasoma Biblia nyumbani kwake.

“Ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima, na aendelee kumwomba Mungu, kwa maana yeye huwapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu; naye atapewa hiyo.” (Yakobo 1:5) Mara nyingi hatufanyi maamuzi mazuri tunapokuwa na mkazo. Ukimwomba Mungu akupe hekima, atakukumbusha kanuni nyingi zinazopatikana katika Neno Lake Biblia zinazoweza kukusaidia.

Nguvu na faraja

Wenzi wa ndoa ambao walikuwa hospitali, wakitembea kwenye bustani. Mume akimsaidia mke wake kutembea kwa kutumia fimbo.

“Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yule anayenipa nguvu.” (Wafilipi 4:13) Akiwa Mungu mweza-yote, Yehova anaweza kukupa nguvu unazohitaji ili kukabiliana na changamoto zako au kuvumilia majaribu unayopitia. (Isaya 40:29) Vilevile, Biblia inamwita Yehova, “Mungu wa faraja yote.” Anaweza kutufariji “katika majaribu yetu yote.”​—2 Wakorintho 1:3, 4.

JE, UTASALI KWA MUNGU?

Ni wazi kwamba Yehova hakulazimishi usali kwake. Badala yake, kwa upendo anakualika ufanye hivyo. (Yeremia 29:11, 12) Namna gani ikiwa unahisi sala zako hazijibiwi? Usikate tamaa. Huenda wazazi wenye upendo wasiwasaidie watoto wao kwa njia ambayo watoto wanataka au kwa wakati ambao wanatazamia. Inawezekana wazazi wana njia bora ya kuwasaidia. Lakini jambo moja ni hakika: Wazazi wenye upendo watawasaidia watoto wao.

Yehova Mungu, mzazi mwenye upendo zaidi anataka kukusaidia wewe pia. Ikiwa utachunguza kwa makini mambo ambayo tumezungumzia kutoka kwenye Biblia, na kujitahidi kadiri uwezavyo kuyatumia, Mungu atajibu sala zako kwa njia bora zaidi!​—Zaburi 34:15; Mathayo 7:7-11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki