Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp21 Na. 3 uku. 15
  • Unaweza Kuamua Maisha Yako ya Wakati Ujao Yatakuwaje

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kuamua Maisha Yako ya Wakati Ujao Yatakuwaje
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUNAWEZAJE KUMPENDA YEHOVA NA KUISIKILIZA SAUTI YAKE?
  • Wakati Wako Ujao, Upo Mikononi Mwako!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
  • Unaweza Kumkaribia Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • “Wapole Wataimiliki Dunia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
  • Utangulizi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
wp21 Na. 3 uku. 15
Mwanamume akiwa mkahawani anamwonyesha rafiki yake kitu fulani kwenye simu.

Unaweza Kuamua Maisha Yako ya Wakati Ujao Yatakuwaje

Miaka 3,500 hivi iliyopita, Yehova Mungu aliwaambia waabudu wake mambo waliyopaswa kufanya ili wawe na maisha bora ya wakati ujao. Alisema hivi: “Nimeweka uzima na kifo mbele yenu, baraka na laana; nanyi lazima mchague uzima ili mwendelee kuishi, ninyi na wazao wenu.”​—Kumbukumbu la Torati 30:19.

Ili wawe na maisha bora ya wakati ujao, watu hao walihitaji kufanya uamuzi sahihi. Leo, sisi pia, tuna nafasi ya kufanya uamuzi unaofaa. Biblia inafafanua jinsi tunavyoweza kuchagua kuwa na maisha bora ya wakati ujao: “Kwa kumpenda Yehova Mungu wenu, kwa kuisikiliza sauti yake.”​—Kumbukumbu la Torati 30:20.

TUNAWEZAJE KUMPENDA YEHOVA NA KUISIKILIZA SAUTI YAKE?

JIFUNZE BIBLIA: Ili umpende Yehova, kwanza, unahitaji kujifunza kumhusu kutoka kwenye Biblia. Utakapofanya hivyo, utatambua kwamba yeye ni Mungu mwenye upendo na anayekutakia mema. Anakualika usali kwake “kwa sababu yeye [anakujali].” (1 Petro 5:7) Biblia inaahidi kwamba ikiwa utajitahidi kumkaribia, ‘naye atakukaribia.’—​Yakobo 4:8.

TUMIA MAMBO UNAYOJIFUNZA: Kumsikiliza Mungu kunamaanisha kufuata mwongozo wake wenye hekima unaopatikana kwenye Biblia. Ukifanya hivyo, “ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.”—Yoshua 1:8.

Ili kujifunza mengi zaidi, tembelea tovuti yetu ya jw.org/sw, ambapo utaweza kusoma Biblia mtandaoni, kupata majibu ya maswali ya Biblia, au kuomba mtu fulani akusaidie kuelewa Biblia bila malipo.

Fanya uamuzi sasa wa kuiruhusu Biblia ikuongoze kuwa na maisha bora ya wakati ujao!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki