Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w24 Desemba uku. 30
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Habari Zinazolingana
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Malaika Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Namna Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
w24 Desemba uku. 30

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

“Malaika waliochaguliwa” wanaotajwa kwenye 1 Timotheo 5:21 ni nani?

Mtume Paulo alimwandikia Timotheo, mzee mwenzake, hivi: “Ninakuagiza kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu na malaika waliochaguliwa, ufuate maagizo haya bila kubagua wala kupendelea.”—1 Tim. 5:21.

Kwanza, tunaweza kuzungumzia malaika hao si nani. Ni wazi kwamba malaika hao si wale 144,000. Ufufuo wa Wakristo watiwa-mafuta kwenda mbinguni haukuwa umeanza wakati mtume Paulo alipomwandikia Timotheo. Mitume na watiwa-mafuta wengine bado hawakuwa viumbe wa roho, hivyo wale “malaika waliochaguliwa” hawawezi kuwarejelea wao.—1 Kor. 15:​50-54; 1 The. 4:​13-17; 1 Yoh. 3:2.

Pia, “malaika waliochaguliwa” hawawezi kuwarejelea malaika ambao hawakutii wakati wa Gharika. Malaika hao walimuunga mkono Shetani na kuwa roho waovu, ambao Yesu aliwapinga. (Mwa. 6:2; Luka 8:​30, 31; 2 Pet. 2:4) Wakati ujao, watafungwa kwenye abiso kwa miaka 1,000 na baada ya hapo wataangamizwa pamoja na Ibilisi.—Yuda 6; Ufu. 20:​1-3, 10, maelezo ya chini.

“Malaika waliochaguliwa” ambao mtume Paulo aliwataja ni lazima walikuwa malaika walio mbinguni ambao walimuunga mkono “Mungu na Kristo Yesu,” ambao wanatajwa kwenye mstari huohuo.

Kuna maelfu kwa maelfu ya malaika waaminifu. (Ebr. 12:​22, 23) Hatupaswi kuwazia kwamba kila mmoja wao ana mgawo uleule kwa wakati uleule. (Ufu. 14:​17, 18) Kumbuka kwamba wakati fulani malaika mmoja alipewa mgawo wa kuwaangamiza wanajeshi Waashuru 185,000. (2 Fal. 19:35) Huenda baadhi ya malaika wana mgawo wa kukusanya “kutoka katika Ufalme [wa Yesu] vitu vyote vinavyosababisha kukwazika na watu wenye mazoea ya kuasi sheria.” (Mt. 13:​39-41) Huenda malaika wengine “watawakusanya watu wake waliochaguliwa” kwenda mbinguni. (Mt. 24:31) Na bado wengine wamepewa agizo la ‘kutulinda katika njia zetu zote.’—Zab. 91:11; Mt. 18:10; linganisha Mathayo 4:11; Luka 22:43.

Malaika akiwaongoza wenzi wa ndoa kwenye nyumba wakiwa katika utumishi wa shambani. Mwanamume aliye ndani ya nyumba akisali.

Inaelekea “malaika waliochaguliwa” wanaotajwa kwenye 1 Timotheo 5:21 walikuwa malaika ambao wamepewa migawo ya pekee inayohusiana na watu wa Mungu. Katika muktadha huo, Paulo alitoa shauri lenye hekima kuhusu wazee, ambao wanastahili kuheshimiwa kutanikoni. Kwa upande wao, wazee wa kutaniko wanapaswa kushughulikia majukumu yao “bila kubagua wala kupendelea” na hawapaswi kufanya maamuzi au kutoa hukumu bila kwanza kufikiria mambo kwa uzito. Sababu moja muhimu ya wao kufuata shauri la Paulo lililoongozwa na roho ni kwamba wanawatumikia ndugu zao “mbele za Mungu na Kristo Yesu na malaika waliochaguliwa.” Hivyo, ni wazi kwamba baadhi ya malaika wamepewa migawo inayohusiana na kutaniko, kama vile kuwalinda watu wa Mungu, kusimamia kazi ya kuhubiri, na kutoa ripoti kwa Yehova.—Mt. 18:10; Ufu. 14:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki