Fundisho la Anasa
◆ Katika kutabiri hali ambazo zingekuwako katika “siku za mwisho,” mtume Paulo alisema kwamba watu wangekuwa “wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.”
Katika kitabu chake What’s the Difference?, mwandishi wa magazeti Louis Cassels anazungumza hedonism, anachosimulia kama “Imani katika Anasa.” Yeye anaandika: “Watu wengi wasioamini kuwako kwa Mungu wanaupata uhakika wao katika shauri juu ya maisha yanayoitwa hedonism (imani ya kwamba anasa ndilo jambo zuri zaidi). Jina hili linatokana na neno la Kigiriki la anasa, na mwanzo wake unarudia huko nyuma kwenye wanafilosofia wa Kigiriki, zaidi Epicurus. Mwenye imani katika anasa anaamini kwamba raha ndilo jambo kuu katika maisha ya kibinadamu.” Kulingana na mwandishi huyu mwenye imani katika anasa anaifuata imani ya kisasa, “Yafurahie maisha yako sana uwezapo kufanya hivyo; utakuwa mfu kwa muda mrefu sana.” Bw. Cassels anaeleza kwamba imani katika anasa ni namna ya dini, na kusema: “Wenye imani katika anasa hawajaona inafaa wakati wo wote kuunda kanisa, ama sivyo kuunda chama cha imani yao. Kwa kweli, wengi wao wanaona inafaa kuzisifu imani nyingine za kidini bure na kushirikiana kwa jina tu na makanisa yanayofurahia fahari katika mtaa. Kwa sababu hii, ni vigumu kukadiria ni wafuasi wangapi waliomo katika dini hii katika Amerika kwa sasa. Lakini hesabu yenyewe bila shaka ni kubwa sana. Nayo inazidi kuongezeka kwa kasi sana.”
Umepaswa mwendo wa Mkristo uwe nini kwa habari ya hii ‘imani katika anasa’? Nyuma ya kusema juu ya “wapendao anasa” na wale walio na ‘mfano wa utauwa lakini wanaokana nguvu zake,’ mtume Paulo aliwaamuru Wakristo: “Hao nao ujiepushe nao.”—2 Tim. 3:1-5.