Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 6/1 kur. 243-244
  • Kujifunza kwa Moyo Njia ya Kujifurahisha ya Wakristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujifunza kwa Moyo Njia ya Kujifurahisha ya Wakristo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Habari Zinazolingana
  • Dokezo la Kujifunza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Msifu Yehova kwa Shangwe Kupitia Nyimbo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Nyimbo Zinazotusaidia Kumkaribia Mungu Zaidi
    Jinsi Michango Yako Inavyotumiwa
  • Mwimbie Yehova Sifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 6/1 kur. 243-244

Kujifunza kwa Moyo Njia ya Kujifurahisha ya Wakristo

KATI ya watu wenye shughuli leo si wengi wenye kazi nyingi kama Mkristo anayeishi kwa uaminifu kulingana na wakf wake kwa Mungu. Kwa sababu ya kuwa na funzo la kipekee la Biblia, kutayarisha na kuhudhuria mikutano mitano ya kundi kila juma, kushiriki katika utumishi wa shambani na katika utendaji mwingine wa Kikristo, ingeelekea kuwa hana saa za kujifurahisha. Kwa hiyo ni wakati gani angefanya jambo la kujifurahisha? Imempasa ajifurahishe, maana kila mtu ahitaji jambo fulani la kujifurahisha.

Lakini hata asipokuwa na wakati wa njia za kawaida za kujifurahisha, anaweza kujifurahisha kwa kujifunza kwa moyo habari za Maandiko? Kwa njia gani? Kwa sababu njia hii ya kujifurahisha hufanya mtu atumie wakati wake asipokuwa na jambo la kufanya, wakati akili yake haifikirii jambo la pekee, kama anapotembea, anapongojea wengine, anapokuwa ndani ya gari la abiria, au anapolala bila kupata usingizi.

Ikiwa ungependa kujaribu njia hii ya kujifurahisha, sababu gani usiianze kwa kujifunza kwa moyo vitabu vile 66 vya Biblia ukifuata jinsi vilivyopangwa​—⁠ikiwa mpaka sasa hujafanya hivyo? Utaona kwamba maarifa hayo yatakusaidia mara nyingi. Je! unamsikiliza msemaji wa watu wote na kuifungua Biblia anapotaja andiko fulani? Usipojua mahali vilipo vitabu vile 66, pengine atamaliza kulisoma andiko kabla hujaliona. Halafu katika kazi yako ya Kikristo ya kuhubiri utaokoa wakati wako mwenyewe na wa wale wenye kukusikiliza, na pia utaonyesha unakifahamu sana Chanzo cha habari zako, kwa kuweza kufungua upesi andiko la Biblia. Unapotembea pamoja na rafiki au mwenzi wako wa ndoa, mnaweza kutaja majina ya vitabu vya Biblia kwa zamu, mmoja baada ya mwingine. Hasa wenye ujuzi wanaweza kusaidia wapya kwa kucheza mchezo huu.a

Halafu yako mambo mengine ambayo mtu aweza kujifunza kwa moyo ajifurahishe. Anaweza kujifunza kufuatanisha siku za uumbaji (Mwa. 1:3 mpaka 2:3); majina ya wana kumi na wawili wa Yakobo (1 Nya. 2:1, 2); kufuatanisha yale mapigo kumi yaliyoipata Misri ya kale kama yalivyopangwa (Kut. 7:19 mpaka 12:30); Amri Kumi (Kut. 20:2-17); wale wafalme 21 wa ukoo wa Daudi kuanza kwa Daudi na kuendelea (1 Fal. 2:12; 2 Fal. 24:18; tazama pia Aid to Bible Understanding, kurasa 340-347); mitume kumi na wawili (Mt. 10:2-4); matunda tisa ya roho (Gal. 5:22, 23) na zile sifa kumi na tano za waangalizi zilizopangwa katika 1 Timotheo 3:1-7.

Pia, ziko sura nyingi sana za Biblia ambazo mtu anaweza kutaja upesi. Haya ni baadhi ya mambo yanayoangaliwa mara kwa mara: Amri Kumi katika Kutoka sura ya 20; Mahubiri juu ya Mlima katika Mathayo sura ya 5 mpaka ya 7 (kutia na Sala ya Bwana ya Kielelezo katika sura ya 6); agizo la Kristo kwa mitume wake kumi na wawili katika Mathayo sura ya 10; unabii wake mkuu katika Mathayo sura ya 24 na 25, Marko 13 na Luka 21; sura inayoeleza vile upendo unavyofanya kazi (1 Kor. 13), na mazungumzo mazuri ya Paulo juu ya ufufuo katika 1 Wakorintho sura ya 15.

Inaweza kuwa faida kubwa Mkristo aliye mtangazaji wa habari njema akiwa na “fahirisi” ya akilini ya habari kuu za Maandiko, kama zile zinazohusiana na jina la Yehova: Kut. 6:3; Zab. 83:18; zinazohusiana na utendaji wa Kikristo wa kuhubiri: Isa. 43:10-12; Mt. 24:14; 28:19, 20; tumaini la Ufalme: Mt. 6:10; Zab. 37:10, 11; Ufu. 21:3, 4; ulizo la kutokuwamo(neutrality): Isa. 2:4; Yohana 18:36; Matendo 5:29; Yak. 1:27; ulizo la damu: Mwa. 9:4-6; Matendo 15:20, 29; alama yenye kutambulisha Wakristo: Yohana 13:34, 35. Ili upate habari zaidi na mitajo ya Maandiko tazama “Make Sure of All Things; Hold Fast to What Is Fine.”

Upande mwingine wenye matokeo kwa Wakristo ni kujifunza kwa moyo maneno yaliyomo katika kitabu cha nyimbo kiitwacho “Kuimba na Kufuatana Wenyewe kwa Muziki Katika Mioyo Yenu.” Watu hujifunza kwa moyo maneno ya nyimbo za kienyeji, nyimbo za kizalendo, nyimbo za mapenzi na nyimbo zipendwazo na watu wengi; sababu gani Wakristo wasijifunze maneno ya nyimbo wanazoimba kama sehemu ya ibada yao? Kujifunza maneno ya nyimbo hizi ni kwepesi zaidi kuliko kujifunza kwa moyo maneno ya Maandiko, kwa maana nyimbo zina vina (sauti za maneno ya mwisho zinapatana). Mawazo mazuri sana yanasemwa katika nyimbo kama vile “Kuishi Kulingana na Jina Letu,” “Uwe Mwenye Kusamehe,” “Sisi Tu Mashahidi wa Yehova!,” “Sasa Ndio Wakati!”, “Kutembea Katika Ukamilifu” na “Asante, Yehova!” Na kwa kuwa ziko sauti za kuimbia maneno hayo mtu anafurahi sana anapoyataja.

Kukionwa kama njia ya kujifurahisha, kujifunza kwa moyo mambo hayo ya Maandiko na nyimbo kunaweza kuleta raha, kunaweza kuwa mchezo, elimu yenye kukufaa kwa utumishi wako wa Ufalme. Kujifunza kwa moyo mambo hayo kisha kuyakumbuka, unapokuwa na nafasi ya kufanya hivyo, kutakusaidia kufikiria sikuzote mambo yenye kutia nguvu imani yako na upendo wako kwa Yehova Mungu,​—⁠Zab. 119:97.

[Maelezo ya Chini]

a Ili upate msaada juu ya jambo hili tazama Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1976

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki