Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 11/15 kur. 527-528
  • Maisha ya Jamaa Yanayofaa—Si Jambo la Zamani Tu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maisha ya Jamaa Yanayofaa—Si Jambo la Zamani Tu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • BABA​—⁠SI MTAFUTA MKATE TU
  • DARAKA LA MAMA
  • KUFANYA MAMBO PAMOJA
  • Bora ya Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Familia—Binadamu Wanaihitaji!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Fanya Bidii ili Kuihifadhi Familia Yako Iingie Ndani ya Ulimwengu Mpya wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Je, Kuna Siri ya Kupata Furaha ya Familia?
    Siri ya Furaha ya Familia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 11/15 kur. 527-528

Maisha ya Jamaa Yanayofaa​—⁠Si Jambo la Zamani Tu

MAISHA ya jamaa yamebadilika sana katika kizazi kilichopo. Wewe umeona badiliko hilo? Je! limetokea katika jamaa yako?

“Nilipokuwa kijana,” kasema mzee mmoja, “sikuzote jamaa yetu ilikula pamoja na ilifurahia kuzungumza nyakati za chakula. Tulitafuta tafrija kama jamaa, tukatembea na kwenda kuvua samaki. Na tulifanya kazi pamoja nyumbani.”

Je! ndivyo ilivyo katika nyumba yako? Katika jamaa fulani leo washiriki hawasemezani sana. Huenda hata wakala nyakati mbalimbali au katika vyumba mbalimbali. Ni nini kilichosababisha uharibifu wa maisha ya jamaa yanayofaa?

Ukuzi wa viwanda ni wa kulaumiwa sana. Siku hizi watu hufanya kazi katika viwanda na afisi, badala ya kufanya kazi nyumbani. Mara nyingi shirika la watu, badala ya jamaa, ndilo huangalia wagonjwa, huelimisha watoto, hutayarisha kingi cha chakula kinacholiwa na watu na hata ndilo huwafurahisha katika mambo ya kujifurahisha. Tena, mkazo wa siku hizi juu ya kujitosheleza kwa mtu mwenyewe hufanya wengi wajitenge na maisha ya jamaa wafuatie miradi au njia zao wenyewe za kujitafutia riziki ya kila siku.

Je! hiyo imeondoa uhitaji wa kuwa na maisha ya jamaa yanayofaa?

“Uchunguzi mpya uliosimamiwa na chama cha hima ya maisha kiitwacho Institute of Life Insurance,” kulingana na habari za mwaka jana, “ulionyesha kwamba 80 kwa mia ya Waamerika waliopita miaka 18 huchagua ‘maisha ya jamaa yenye furaha’ kama mradi wao namba moja. Maisha ya jamaa yenye furaha yalipendelewa kuliko ‘nafasi ya kuwa na maendeleo kama mtu’ . . . ‘njia ya kujitafutia riziki yenye kutosheleza’ . . . na ‘kuchuma pesa nyingi sana.’”

Je! maisha ya jamaa yanayofaa ni mradi wa maana kwako? Waweza kuyapataje? Na tuangalie madaraka fulani makubwa ya washiriki wa Jamaa.

BABA​—⁠SI MTAFUTA MKATE TU

Watu wanaochunguza tabia ya kibinadamu hukazia-kazia ubora wa daraka la baba katika maisha ya jamaa. “Uchunguzi zaidi na zaidi,” asema mwandikaji Ana Honig wa chama kiitwacho Women’s News Service, “wahakikisha kwamba vijana wasiokuwa na baba zao mara nyingi wanaweza kudhoofika sana moyoni.”

Je! wewe ni mume na baba? Bila shaka unaipenda sana jamaa yako. Huenda hata ukajikaza sana sana ukijaribu kuwapa chakula, mahali pa kukaa, mavazi na starehe nyingine. Lakini ikiwa hivyo tu ndivyo wewe hufanyia jamaa yako, huenda ukawa unafanya kosa kubwa. Sababu gani? Angalia barua aliyoandikiwa mwandikaji wa safu za magazeti na kivulana wa miaka kumi na mitatu:

“Nyakati nyingine natamani [baba yangu] anipigie kelele, ili nijue anajali. Nikitaka kwenda ko kote au kufanya jambo, naambiwa niulize mama. Baba husema kazi yake ni kuleta pesa. Ningependa kuwa na baba mwenye kuketi na kusema nami, mwenye wakati wa kutembea porini nami au ko kote tu. Baba hajali hata nikipata maksi ya chini zaidi. Yeye husema, ‘Mpelekee mama yako akayaangalie!’”

Biblia, pia, yakazia uhitaji wa akina baba kupendezwa wenyewe na watoto, ikisema: “Ninyi, akina baba, msiwe mkiwaudhi watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika adabu na rekebisho la moyoni la Yehova.” (Efe. 6:4, NW) Je! wewe unalifahamu Neno la Mungu kutosha kuweza kuwapa wazao wako hilo “rekebisho la moyoni”?

DARAKA LA MAMA

Daraka la mama ni la maana sana pia. Zaidi ya kufanya kazi nyingi sana za kinyumbani, kwa kawaida mama huwa na watoto wake wakati mwingi wa kila siku. Akionyesha uanana na uchangamfu anaposhughulika na watoto wake, na kuwatia moyo watendeane ivyo hivyo, itakuwa vigumu sana kwa watoto kutaka kuiacha hali hiyo yenye upendo ya jamaa wafuate njia zao.

Akieleza juu ya daraka la mke katika maisha ya jamaa yanayofaa, Theodore R. Van Dellen, M.D., aandika hivi katika safu yake isemayo “Daktari wa Jamaa”:

“Mke mwema hufanya nyumba iendelee kuwa tulivu na yenye starehe na upendo na kutumainiana husitawi humo. Ajua kwamba maono ya moyoni na akilini ya maisha ya ndoa ni ya maana ili mumewe na watoto wawe na hali njema. . . .

“Hana uwezo wa kuzuia hali zisizopendeza huko kazini, lakini anasimamia nyumbani. Uwe naye [mume] muda mwingi iwezekanavyo kwa kutokubali ukaribishaji mwingi mno wa kuwa na marafiki. Msaidie [mume] apange na aufurahie wakati wake wa starehe. . . . Uwe msikilizaji mwenye huruma anapokueleza matatizo yake.”

Vijana wanaweza kutimiza daraka lao, pia, hasa kwa kushirikiana na wazazi wao wanapoombwa wafanye mambo. Kumbukeni shauri la Maandiko: “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.” (Kol. 3:20) Kanuni njema ya Maandiko ya kuwa na maisha ya jamaa yanayofaa ni hii: “Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake.”​—1 Kor. 10:24.

KUFANYA MAMBO PAMOJA

Walakini, ili maisha ya nyumbani yawe ya kufurahisha zaidi sana, lazima washiriki wa jamaa wafanye mambo pamoja. Washiriki wa jamaa wanaweza kufanya nini pamoja katika jiji ambamo viwanda vimefanya jamaa zifanye kazi zaidi humo? Angalia mambo machache ambayo baba mmoja wa New York mwenye vivulana wawili aliona yakifaulu:

“Tangu walipokuwa wadogo kabisa mimi na mke wangu tuliwafundisha vivulana jinsi ya kufanya mambo nyumbani. Nimeona kwamba vijana hao wana nia hata ya kufanya kazi chafu-chafu, kama kusafisha choo, wakituona sisi tukifanya mambo kama hayo.

“Wakati vivulana walipotimiza umri wa kutosha kuweza kuwa na ufahamu, niliwapeleka kwenye sanduku lenye vyombo vya matumizi mbalimbali. Nikawaeleza kila chombo ni cha kazi gani na jinsi ya kukitumia. Sasa wanafurahia kufanya kazi ndogo ndogo za nyumbani.”

Je! wewe hutia moyo washiriki wa jamaa yako wafanye kazi pamoja hivyo? Walakini, kazi peke yake siyo inayoleta maisha ya jamaa yanayofaa. Baba aliyetajwa juu aendelea kusema hivi:

“Kila mtu huhitaji burudisho. Tumeona inafaidi kuwa na tafrija pamoja kadiri iwezekanavyo. Kwa mfano, katika New York yako mambo ya namna nyingi yanayoweza kufurahiwa bila kulipa pesa au kwa kulipa pesa kidogo. Mara nyingi sisi hutembea kwa miguu kwenye bustani za miti na mimea ya uchunguzi wa elimu au bustani ya kawaida kucheza mpira. Nyakati nyingine sisi hutumia wakati tukichunguza-chunguza vitabu katika muduka ya vitabu, tukienda nyumba za vitu vya kihistoria vilivyohifadhiwa (museums) au kwenye machezo ya kuchekesha yanayoonyeshwa bure.

“Bila shaka, si lazima jamaa itoke nje ndiyo ikafurahie tafrija pamoja. Nyakati nyingine sisi huketi na kusoma Biblia pamoja au vitabu vingine vizuri kama vitabu vya mambo ya kale ya Kigiriki na Kirumi. Hivi majuzi vivulana wangu na mimi tulijenga gari la farasi pamoja. Ilituchukua muda mrefu na kulikuwa na migogoro fulani. Lakini tulipendezwa tulipoona likianza kufaa na tulipolitazama baada ya kulimaliza, tukijua kwamba tulilitengeneza kwa mikono yetu wenyewe. Utendaji kama huo husaidia watoto, wasitake kuwa nje wakifanya matata pamoja na waasi.”

Je! wewe hutumia kwa faida nafasi za kufanya mambo pamoja na jamaa yako? Maelfu ya jamaa ulimwenguni mwote yameona kwamba kutumia kanuni za Biblia, kama zilizotangulia kutajwa, kumeleta furaha kuu zaidi katika jamaa zao. Wewe ungetaka kujua jinsi ya kutumia mashauri ya Maandiko kwa jamaa yako mwenyewe? Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia kujifunza nawe Biblia bila malipo nyumbani kwako au mahali po pote pafaapo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki