“Kama Mwiba”
“Kama mwiba uingiao katika mkono wa mlevi,” yasema Mithali 26:9, “kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.” Mtu aliyelewa aweza kujiumiza mwenyewe au wengine kama kwamba kwa kutumia mwiba. Vivyo hivyo, mtu asiye na ufahamu aweza kuumiza watu kwa kutumia mithali vibaya, akiitumia kwa njia isiyofaa.