Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 1/1 uku. 23
  • Sababu Gani Hua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Gani Hua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Gharika Kuu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Yohana Anambatiza Yesu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 1/1 uku. 23

Sababu Gani Hua?

Mara Yesu alipokwisha kubatizwa katika maji, “[roho takatifu ikashuka] juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua.” (Luka 3:22) Labda kushuka huku kwa roho kulifananishwa na kupigapiga kwa mabawa ya hua au njiwa anapokaribia kituo chake.

Hua au njiwa walitumiwa na Waisraeli wa kale kwa makusudi ya dhabihu. (Marko 11:15; Yohana 2:14-16) Ndege huyo alifananisha hali ya kutokuwa na hatia na hali ya kutokuwa na uchafu, kama aliyeachiliwa na Nuhu kutoka safinani aliyerudi akiwa na jani la “Iweni . . . wapole kama hua” au njiwa. (Mt. 10:16) Alikuwa njiwa aliyeachiliwa na Nuhu kutoka safinani aliyerudi akiwa na jani la mzeituni, kuonyesha kwamba maji ya gharika yalikuwa yakipunguka. (Mwa. 8:11) Hii ilionyesha kwamba wakati wa pumziko na amani ulikuwa karibu, kwa maana ilikuwa imetabiriwa kwa habari ya Nuhu hivi: “Huyu ndiye atakayetufariji kwa kazi yetu na kwa taabu ya mikono yetu katika nchi aliyoilaani [Yehova].” (Mwa. 5:29) Basi, wakati wa kubatizwa kwa Yesu, yule hua au njiwa aliweza kuvuta fikira kwa kufaa kwenye daraka la Yesu kama Masihi, Mwana wa Mungu aliye safi na asiye na dhambi. Na kutoa kwake uhai kwa ajili ya wanadamu kuliweka msingi wa kipindi cha pumziko na chenye amani wakati wa utawala wake kama ufalme.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki