Mwenendo Mwema Waunganisha Jamaa
WATU wanapoanza kugeuza maisha zao wakizipatanisha na mapenzi ya Mungu, washiriki wa jamaa hawaoni maana nzuri mara hiyo. Walakini, labda mwishowe wanaweza wakaona ubora wa mageuzi yenye faida ya mtu nao waanze kujifunza Biblia.
Haya yalikuwa ndiyo maono ya mwanamume mmoja katika Jamhuri ya San Marino. Mazoea yake mabaya yaliharibu maisha yenye furaha ya nyumbani. Pahali pa kutumia wakati akae na jamaa yake mara nyingi alikuwako kwenye nyumba ya pombe jioni. Alipoona ubaya wa maisha yake, alimwomba Mungu amsaidie kuacha mazoea yake mabaya. Mwisho, alipokuwa katika kumtembelea mama yake siku moja, akajua kwamba alikuwa akijifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Alianza kuhudhuria funzo hili, lakini kufanya hivi kulitokeza upinzani wa jamaa. Mke wake hakupendezwa na yale aliyokuwa akijifunza. Mke huyu hata alionya kwamba atamwacha achukue na watoto.
Ndipo, siku moja, mwanamume huyu alianza kugombana na baba yake mkwe juu ya mambo ya jamaa. Baba yake mkwe alikasirika hata akampiga mkwewe ngumi. Ijapokuwa mkwe alijua yeye mwenyewe hakuwa na kosa, hakulipa kisasi. Alimsamehe baba mkwewe bila kuwa na kinyongo juu yake. Mke alipovutwa na mwenendo wa mumewe katika jambo hili, alianza kuchunguza imani ambayo mumewe alikuwa ameikubali. Mke alianza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova. Akieleza yaliyofuata hapo, mume anasema: “Nikaanza funzo la Biblia pamoja na watoto na mke wangu, na ni furaha kuona maendeleo yake na namna tulivyo jamaa iliyoungana sasa.”