‘Husaidia kuwa miongozo kwa maisha ya kila siku’
HIVYO ndivyo mwanamke mmoja wa kutoka Toronto, Kanada, alivyoita vichapo vya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti. “Mimi huona shangwe kuvisoma na huziona habari hizo kuwa zenye kuarifu sana, zenye kuchangamsha moyo, na juu ya yote, zenye kusaidia sana kuwa miongozo kwa maisha ya kila siku.”
Aliongeza hivi: “Mimi ni mhitimu wa chuo kikuu, na ni lazima nikiri kwamba ni ajabu sana kwamba nimejifunza mengi zaidi kupitia vichapo vyenu kuliko kupitia miaka yangu yote ya kujifunza. Hasa nilionea shangwe kitabu chenu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Hakuna vichapo vinginevyo ambavyo vimeweza kuwa na matokeo chanya yenye uzito wa kadiri hiyo juu ya maisha yangu kama hivyo vyenu—vimenisaidia sana sana; nami nawatolea asante kikweli kwa jambo hilo.”
Kitabu kilichotajwa juu, Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha, hutoa madokezo hususa ambayo husaidia kutatua matatizo na kufanya ndoa ipendeze kama vile Muumba alivyoikusudia. Ili upate nakala yako, jaza na utupelekee hati yenye anwani iliyopo chini pamoja na mchango wa Kshs. 20/= (Tshs. 150/=; RWF 100).
Tafadhali nipelekeeni kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192, Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Mimi nawapelekea Kshs. 20/= (Tshs. 150/=; RWF 100).