Kuchoshwa Kwaweza Kusababisha Mkazo na Kushuka Moyo
KUCHOSHWA kwaweza kuwa mmoja wa mikazo yenye kuponda, kuumiza zaidi ambayo wanadamu wanaweza kupatwa nayo.” Aripoti hivyo Dakt. Jay Shurley, aliyepewa heshima kuwa profesa wa saikayatri na sayansi za kitabia kwenye Chuo Kikuu cha Oklahoma, katika makala fulani katika gazeti Elle. “Kuchoshwa,” akasema, “Ni hisia isiyo ya kustarehesha, isiyopendeza kwamba kuna jambo lenye kasoro na maisha zetu. Ni ombi la kichocheo cha aina fulani, ishara kwamba mahitaji yetu hayatimizwi, hisia ya kunaswa. Kuna mkazo sana, na kwaweza kuongoza kwenye matatizo mbalimbali—kushuka moyo, matumizi ya dawa za kulevya, maradhi yanayojumuisha akili na mwili, au jambo rahisi kama kulala mno ili kuepuka kuchoshwa.”
Utafiti wa Dakt. Shurley juu ya visababishi na matokeo ya kuchoshwa ulikuwa ni sehemu ya kazi ya miaka mitano katika Antarktiki. Moja la mawazo yake yenye kushtua zaidi lilikuwa kwamba kuchoshwa kwaweza kutokeza mzunguko wenye kufululiza. Kunaweza kusababisha mkazo mkubwa katika mtu. Nao mkazo waweza kusababisha kuchoshwa ambako nako kunasababisha mkazo zaidi wa kindani.
Matokeo ya mzunguko huo wa mkazo wa kuchoshwa yaweza kudhuru sana. Dakt. Shurley anadai: “Talaka nyingi zinatokana na mume au mke mwenye kuchoshwa na kazi yake, kuchoshwa sasa kwa kuwa watoto wameenda zao, kushoshwa na maisha yasiyochangamsha ya kijamii, lakini ni nani ambaye hawezi au hataweza kukabili uhakika wa kwamba tatizo hill kwa msingi ni la kibinafsi.” Kwa hiyo mwenzi huyo aliyechoshwa anataliki na “kutafuta mtu mwingine mpya, na kwa kitambo hilo linatatua tatizo lake. Kwa kitambo. Halafu mambo yanarudia palepale.” Ndiyo, kuchoshwa kwa mara nyingi kunamtumbukiza mtu huyo katika mfadhaiko.
“Akili ya kibinadamu,” akasema Dakt. Shurley, “ina njaa ya badiliko, kitu cha kung’ang’aniwa, kujifunza, na mambo mapya. Kuwa na mambo mbalimbali si ndiko kunakokoleza maisha. Ndiko msingi wa maisha.” Kwa habari hiyo, Dakt. Shurley alieleza ni kwa nini matajiri wana matatizo ya pekee ya kuchoshwa. “Wanaweza kupata karibu kila kitu wanachotaka. Lakini ili jambo liridhishe kikweli, lazima lifanyiwe kazi, lifanyiwe kazi ili lifikiwe. Inapokuwa hakuna kitu cha kung’ang’aniwa kikweli, hata maisha yenye msisimuko zaidi, yenye mapendeleo mazuri zaidi yanachosha—ambayo ni sababu moja watu wengi sana katika hali hiyo wanageukia matumizi ya dawa za kulevya.”