Wakaaji wa Nje ya Dunia Hii—Kupata Jibu
SIKU ya Februari 17, 1600, mwanamume mmoja jina lake Giordano Bruno aliteketezwa hai katika uwanja wa watu wote katika Roma, Italia. Kwa nini? Miandiko yake ilikuwa imeudhi kanisa. Miongoni mwa mambo mengine, alifundisha kwamba kulikuwako malimwengu mengi yenye kukaliwa katika ulimwengu wote mzima. Huko nyuma katika karne ya 11, kanisa lilikuwa limejulisha rasmi kwamba fundisho hilo, wingi wa malimwengu, ni uzushi. Kulifundisha kulikuwa kufa. Bruno alikufa.
Mpaka karne ya 19, mjadala juu ya kama kuna uhai katika malimwengu mengine uliendeshwa katika dini. Kwa karne nyingi, viongozi wa kidini na wanasayansi wenye kuwa chini ya uvutano wao walisisitiza kwamba dunia ilikuwa ndicho kitovu cha ulimwengu wote mzima; kwamba ulimwengu wote mzima uliumbwa katika 4004 K.W.K.; na kadhalika.
Basi, si ajabu sana kwamba wanasayansi wengi na wengine hawastahi dini sana. Ingawa hivyo, katika kufanya hivyo wengi wamepoteza staha yao kwa Biblia pia, wakiwazia kwamba hiyo ndiyo iliyokuwa chanzo cha dhana zote hizo zenye makosa. Hiyo haikaribii ukweli kamwe.
Biblia haidai kuwa kitabu cha masomo ya sayansi. Hata hivyo, haikosi kamwe usahihi igusiapo habari ya ulimwengu wote mzima au jambo lolote la kisayansi. Kwa kielelezo, Biblia haisemi kamwe kwamba dunia na binadamu ndio kitovu cha ulimwengu wote mzima. Bali, waandikaji wayo waliovuviwa walionyesha uelewevu wa wazi juu ya jinsi mwanadamu alivyo duni akilinganishwa na kosmosi iliyo kubwa sana.—Zaburi 8:3, 4.a
Kwa hiyo, basi, kulingana na Biblia, je! kuna mtu yeyote huko nje?
Biblia Hujibu
Kulingana na Biblia, si kwamba tu kuna uhai nje ya dunia hii bali uko kwa wingi. Ni wenye kutatanisha zaidi, wenye kupendeza zaidi, na wenye kuaminika zaidi ya chochote ambacho wanamageuzi, waandikaji wa hadithi-ubuni za kisayansi, na watayarisha-sinema wamepata kuota juu yacho. Ingawaje, mkaaji wa nje ya dunia hii ni mhai tu ambaye asili yake ni nje ya dunia hii na halianga yayo.
Wanasayansi hushangaa kama kungeweza kuwa kuna namna za uhai zisizoweza kugunduliwa kwa uwezo wetu. Biblia hutuhakikishia kwamba kwa kweli kuna wahai wa jinsi hiyo. Lakini hawakutokana na mageuzi. Kama vile uhai wote katika ulimwengu wote mzima, uwe wa umbo lolote lile, wao walitoka kwa Chanzo cha uhai, Yehova Mungu. Yeye ni Mhai wa roho, naye ameumba mamiriadi ya wahai wengine wa roho wa namna tofauti-tofauti: malaika, makerubi, na maserafi. Wao hufanya kazi kazi na utendaji tofauti-tofauti katika tengenezo lake la kimbingu lenye utataniko wa vitu vingi.—Zaburi 104:4; Waebrania 12:22; Ufunuo 19:14.
Namna Gani Juu ya Uhai Katika Sayari Nyinginezo?
Watu fulani walio mashuhuri kidini wamesisitiza kwamba Mungu hangeumba ulimwengu wowote bila kusudi na kwamba kwa sababu hiyo ni lazima malimwengu yote yanayokalika yakaliwe. Je! Biblia husema hivyo? Sivyo. Biblia huonyesha kwamba kwa kadiri kubwa haielekei kwamba kufikia hapa Mungu ameumba viumbe wa kimwili wenye akili katika sayari nyingine zozote isipokuwa yetu wenyewe. Jinsi gani hivyo?
Ikiwa Mungu aliumba wahai hao, alifanya hivyo kabla hajaumba Adamu na Hawa. Wahai hao walibaki wakiwa waaminifu kwa Muumba wao, au kama vile Adamu na Hawa, wakatenda dhambi na kuanguka ndani ya kutokamilika.
Lakini ikiwa walipata kuwa wasiokamilika, walihitaji mkombozi. Kama vile mtunga-insha mmoja alivyoweka wazo hilo: “Mtu huwa na wazo hili lenye kuhofisha sana kwamba siku ya Ijumaa [siku ambayo Yesu Kristo aliuawa], kila Ijumaa, mahali fulani katika ulimwengu wote mzima Yesu anaangikwa juu kwa ajili ya dhambi za mtu fulani.” Lakini hilo si jambo la Kimaandiko. Biblia hutuambia kwamba Yesu ‘alikufa kuhusu dhambi mara moja kwa wakati wote.”—Warumi 6:10, NW.
Namna gani kama wahai hawa wangalibaki wakiwa wakamilifu? Naam, Adamu na Hawa walipotenda dhambi, kwa kweli wao walikuwa wakitia shaka juu ya kufaa kwa Mungu kutawala juu ya ulimwengu wa wahai wa kimwili wenye akili. Kama wakati huo kungalikuwa kuna sayari nyingine, ulimwengu wenye kujaa wahai wa kimwili wenye akili wakiishi kwa upatano na kwa uaminifu-mshikamanifu chini ya utawala wa Mungu, je! wasingaliitwa waje kuwa mashahidi wa kushuhudia kwamba utawala wa Mungu hufanya kazi kikweli? Yaonekana haiepukiki kukata shauri hivyo, kwa kuwa tayari yeye ametumia hata wanadamu wasiokamilika wawe mashahidi kwa ajili ya suala lilo hilo.—Isaya 43:10.
Basi, je! hiyo yamaanisha kwamba Mungu aliumba hayo mamilioni yasiyohesabika ya majua (na sayari ikiwa ziko) bila kusudi lolote? Sivyo hata kidogo. Ingawa, kwa kufikiria hali ya Yesu Kristo isiyo na kifani, twajua kwamba dunia ndiyo sayari pekee inayokaliwa sasa hivi katika ulimwengu wote mzima, na ingawa pia twajua kwamba itasimama milele ikiwa bila kifani kama sayari ambapo Muumba alitetea ufaaji wa utawala wake, hatujui ya wakati ujao.
Hatuko Peke Yetu
Siku baada ya siku, mwaka nenda mwaka rudi, wanaanga wa SETI huendelea kuzichungua-chungua anga ili wapate ishara kutoka kwenye uhai wenye akili. Wao huhisi kwamba huenda utafutaji wao ukachukua mwongo mwingine, au huenda ukachukua karne moja. Lo, kinyume gani hicho! Wanatumia maisha zao, matumaini yao, na mapesa mengi wakitafuta ishara ambayo ainabinadamu ilipokea karne nyingi zilizopita. Hiyo ni kwa sababu Biblia yenyewe ni ujumbe kutoka kwa Mkaaji Mwenye Akili wa nje ya dunia hii, nayo ni bora kwa kila njia kuliko ishara ambazo huonwa na hata wanasayansi walio na matazamio mazuri zaidi.—Ona sanduku katika ukurasa 10.
Ainabinadamu imeitikiaje ujumbe pekee ulio halisi kutoka nje ya dunia hii? Wanadamu, kwa ujumla, huiitikiaje Biblia? Wao huipuuza. Huitumia vibaya kimakusudi ili kutimiza malengo yao wenyewe. Wao humvunjia heshima Aliyeipeleka kwa unamna-namna wa mafundisho yasiyo na msingi na yenye hofu za kishirikina. Wao hata huiita udanganyifu na kukana kuwako kwenyewe kwa Aliyeipeleka. Ni wazi kwamba Muumba wetu hakupendezwa hata kidogo na itikio la wanadamu. Hata hivyo, yeye ameendelea kuwasiliana. Kwa njia ya Neno lake, anaelimisha mamilioni ya watu leo katika njia za amani. Watu hawa huwakilisha Yehova na kuupelekea ulimwengu mawasilisho yake. Lakini ni wachache sana kati ya ainabinadamu ambao huwasikiliza. Ulimwengu kwa ujumla hugeuza sikio la uziwi.—Isaya 2:2-4; Mathayo 24:14.
Ingawa hivyo, jambo la kufurahisha ni kwamba kila mmoja wetu aweza kuwasiliana na Mhai huyo aliye mkubwa zaidi katika ulimwengu wote mzima, tena bila tekinolojia yenye gharama kubwa, bila kungoja sana ili jumbe zivuke ile nafasi kubwa ya anga. Wewe waweza kusikiliza sasa kwa kujifunza Biblia yako na kujithibitishia mwenyewe kama kweli yatoka kwenye Chanzo chenye nguvu kupita binadamu. Waweza kuitikia kwa sala na kwa njia ambayo waishi maisha yako. Sisi hatuko peke yetu. Muumba wetu huahidi kwamba yeye “hawi mbali na kila mmoja wetu.”—Matendo 17:27; ona pia 1 Nyakati 28:9.
Wala yeye hajamaliza kuwasiliana na wanadamu. Ameahidi kubadili sana sana mwendo wa historia ya ulimwengu, kumaliza ile mbio-mbio ya ainabinadamu kuelekea kujiangamiza yenyewe kwa kuubomoa kabisa huu mfumo wa mambo usioweza kufanya kazi na mahali pao aweke serikali atakayofanyiza mwenyewe, moja ambayo itafanya kazi kikweli kwa faida ya wote. (Danieli 2:44; Isaya 9:6, 7) Ndiyo, uwasiliano ule utakaofuata kutoka kwa Mwenye Akili aliye mkubwa zaidi wa nje ya dunia hii waahidiwa kuja kwa namna ya kitendo, si maneno.—2 Wathesalonike 1:6-9.
[Maelezo ya Chini]
a Kwa uthibitisho wa kwamba Biblia hupatana na sayansi iliyothibitishwa, tafadhali ona kitabu The Bible—God’s Word or Man’s? chenye kuchapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.
[Sanduku katika ukurasa wa 10]
Jumbe Ambazo Wanasayansi Ujumbe Ambao Wao Hupuuza
Wanatumainia Kupata Katika —Neno la Mungu, Biblia:
Utafutaji Wao wa Watu Wenye
Akili Wanaokaa Nje ya Dunia Hii:
*Zingeweza kuwa ni ishara bandia, *Hutoka kwa Mwenye Akili
kwa kuwa hutukia kwa kawaida; mwenye nguvu zipitazo za
viini-macho vyaweza kufanywa. kibinadamu aliye mkaaji wa nje ya dunia hii.
*Zingeweza kutoa elimu na manufaa *Sasa hivi unaandaa elimu
za mamilioni ya miaka ya ujuzi. kwa ajili ya mamilioni,
ukiwa na manufaa za hekima iliyo ya
umri mkubwa kuliko ulimwengu wote
mzima.—Ayubu 36:26; Zaburi 103:14;
*Zingeweza kutufundisha kuepuka *Yawafundisha amani mamilioni
teketezo la kinyukilia na vita vyote. ya watu sasa hivi;
Mtungaji wao aahidi kuhifadhi dunia
milele na kuharibu wale
wanaoiharibu.—Zaburi 104:5;
*Zingeweza kutoa maponyo kwa *Mtungaji wao ameonyesha uwezo
magonjwa na hata kifo; kifo wake kuponya magonjwa yote;
cha aksidenti tu ndicho kingebakia. aahidi kumaliza kifo na pia
kutangua matokeo yacho, akileta uhai
wa milele.—Luka 7:22; Yohana
20:30, 31; Ufunuo 21:4.
*Zingeweza kumaliza ‘upweke wa *Sasa hivi Mtungaji wa Biblia
kikosmosi’ wa ainabinadamu. “hawi mbali na kila mmoja
wetu.”—Matendo 17:27.
*Huenda zisiweze kutafsiriwa; *Wapatikana kwa urahisi kwa
ingechukua maelfu—labda mamilioni— familia ya kibinadamu. Sisi
ya miaka kujibu na kufanya maongeo. twaweza kuusoma sasa na
kuuitikia. Jumbe zetu hupokewa mara
ile ile.—Yohana 17:3;
*Msingi wa yote yaliyo juu ni *Msingi wa imani yetu katika
kukisia-kisia na kudhania-dhania. yaliyo juu ni uthibitisho
na akili nzuri.—Waebrania 11:1.
[Picha katika ukurasa wa 11]
Sisi twaweza kuwasiliana na Mhai aliye mkubwa zaidi katika ulimwengu wote mzima