Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g91 11/8 kur. 19-21
  • Je! Nitakuwa Mtu wa Kawaida Nikiwa na Mzazi Mmoja Tu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Nitakuwa Mtu wa Kawaida Nikiwa na Mzazi Mmoja Tu?
  • Amkeni!—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu Nyumba Zenye Mzazi Mmoja Zipo
  • Nyumba Zilizovunjika—Maisha Yaliyovunjika?
  • Kushinda Maoni Mabaya
  • Kuziona Manufaa
  • Ninaweza Kuwa na Furaha Katika Familia ya Mzazi Mmoja?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Nawezaje Kuwa na Furaha Nikiishi na Mzazi Mmoja Tu?
    Amkeni!—1992
  • Familia za Mzazi Mmoja Zaweza Kufanikiwa!
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Mzazi Mmoja, Matatizo Mengi
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1991
g91 11/8 kur. 19-21

Vijana Wanauliza. . .

Je! Nitakuwa Mtu wa Kawaida Nikiwa na Mzazi Mmoja Tu?

KABLA ya kufika miaka yao ya 18, zaidi ya nusu ya watoto katika United States watatumia sehemu ya miaka yao kwenye nyumba ya mzazi mmoja. Kwa sasa, vijana milioni 12—1 kati ya 5 katika United States—tayari wanafanya hivyo. Familia ya mzazi mmoja imebandikwa jina, “mtindo wa kifamilia unaokua kwa haraka zaidi” katika United States. Takwimu za mataifa mengineyo zikiwa hazifuati kwa umbali sana, hiyo huenda ikathibitika kuwa kweli tufeni pote.

Mweneo wa familia zenye mzazi mmoja umepunguza mno aibu iliyozilemea katika nyakati zilizopita. Bado, kama vile kijana mmoja aelezavyo, vijana wengi wanahitaji “kupunguza maoni mengi” ili kukabiliana na maisha katika nyumba yenye mzazi mmoja. Wengine hata huhofu kwa vyovyote watakuwa na vizuizi au wasio wa kawaida kwa sababu ya kuwa na mzazi mmoja tu nyumbani. Je! hofu za namna hiyo ni za sababu nzuri?

Sababu Nyumba Zenye Mzazi Mmoja Zipo

Wachache watakanusha kwamba kuwa na baba na mama wenye upendo kwenye nyumba ni hali iliyo bora kabisa. Muumba wetu alikusudia iwe hivyo. (Mwanzo 1:27, 28) Waefeso 6:1 inaendelea kudhihirisha hiyo inaposema: “Enyi watoto watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. Waheshimu baba yako na mama yako.”

Lakini kwa sababu moja au nyingine, huenda ukanyimwa hali hiyo iliyo bora kabisa. Kwa sababu ya tukio lisilotazamiwa, huenda mmoja wa wazazi wako akafa. (Mhubiri 9:11) Misiba kama hiyo ilitukia hata katika nyakati za Biblia, neno “yatima” likionekana mara 40 katika Maandiko. (Linganisha Kumbukumbu 24:19-21.) Au huenda mmoja wa wazazi wako akakosekana kwa muda kwa ajili ya kuajiriwa kazi ng’ambo. Kwa upande mwingine, hali nyinginezo, kama vile ukosefu wa uaminifu kwa viapo vya ndoa, huenda ukasababisha wazazi wako kuachana au kutaliki. (Mathayo 19:3-6, 9) Huenda ikawa mama yako, kabla ya kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, alipata mimba akiwa hajaolewa akachagua kukulea peke yake.

Katika tukio lolote, wewe huna amri yoyote juu ya hali ya ndoa ya wazazi wako, wala hakuna sababu yoyote kwako kulemewa na hatia hivi kama ni wewe ndiye mwenye kulaumiwa; wala huhitaji kuona aibu ikiwa ulizaliwa nje ya kifungo cha ndoa. Ikiwa mama yako ni mtumishi aliye wakfu wa Yehova Mungu, makosa yake ya wakati uliopita yamekwisha kusamehewa zamani. (Linganisha Waefeso 2:2, 4.) Na hata kama hajamwuliza Mungu msamaha wake, hiyo haizuii wewe kuwa safi machoni pa Mungu.—1 Wakorintho 8:3.

Ni kweli, kukua katika familia yenye mzazi mmoja huenda ukakabili matatizo na majaribu ya namna ya pekee. Lakini, kama vile kitabu How to Live With a Single Parent kinavyoonelea: “Mengi ya magumu watoto [wenye mzazi moja] waliyo nayo . . . huenda yakatokana na mfano walio nao ulio mbaya na wenye kujiangamiza, wa wao wenyewe.” Kuwaza kubaya kama huko kunatokea wapi, nawe waweza kukuondoleshaje?

Nyumba Zilizovunjika—Maisha Yaliyovunjika?

‘Wazao wa nyumba iliyovunjika,’ ‘familia iliyogawanyika,’ ‘nusu familia,’ ‘familia iliyoganduliwa’—labda umesikia mibandiko mibaya hiyo ikitumiwa kwa familia yako. Na ijapokuwa hufanywa yasiwe makali sana kwa kutumiwa mara kwa mara, maelezo kama hayo bado yaweza kusababisha uchungu.

Njia ambayo wengine hukutendea yaweza pia kuchochea maoni mabaya kuhusu familia yako. Kwa mfano, walimu wengine, wameonyesha wazi mtazamo mbaya usio wa wepesi wa kuona hisia za wengine kuelekea wanafunzi wenye mzazi mmoja. Wengine hata wamejulikana kudhania kwamba vijana kama hao kwa kawaida huwa na maisha ya familia isiyo ya kawaida nao ni wepesi kulaumu mazingira yao ya nyumbani kwa tatizo lolote la kitabia. Kufanywa daima uone kwamba familia yako si ya kawaida kwaweza kwa kufaa kukujaza na mahangaiko kuhusu hali njema yako ya maoni ya moyoni.

Lakini je! mara kwa mara unakuwa katika hatari ya kuwa duni kiakili na katika maoni ya moyoni kwa sababu tu unaishi kwenye nyumba yenye mzazi mmoja? Hata kidogo! Journal of Marriage and the Family lilikiri kwamba “kupoteza mzazi huenda kukaleta kipindi cha usitawi wa polepole” mwanzoni. Hata hivyo, hicho mara nyingi “hufuatwa na wakati ambapo mtoto awafikia marika au hata kuwapatia.” (Italiki ni zetu.) Makala hiyo ilimalizia hivi: “Wazo tu lenye kutia mambo mengi kwamba familia yenye mzazi mmoja kwa kawaida huwa na matokeo mabaya, yenye kudumu juu ya watoto wote si la haki.” Makala nyingine katika gazeti lilo hilo iliripoti vivyo hivyo kwamba uchunguzi “haliungi mkono hata kidogo wazo kwamba ‘nyumba zilizovunjika hutokeza maisha machanga yaliyovunjika.’”

Hata iwapo mambo ya hakika ya namna hiyo huenda yakawa yenye kitia moyo wa kadiri fulani, maoni mabaya huenda bado yakatokea mara kwa mara. Unaweza kupiganaje nayo kwa kufanikiwa?

Kushinda Maoni Mabaya

Hatua ya kwanza ingekuwa kujifunza kukubali hali yako. Ni kweli, huzuni na maoni ya kuwa umepoteza ni ya asili ikiwa wazazi wako wametaliki au ikiwa mzazi mpendwa amekufa. Sarah mwenye umri wa miaka kumi na mitatu ambaye wazazi wake walitaliki wakati alipokuwa na miaka kumi, apendekeza hivi: “Usifikiri hali yako mno, kuwa na hali ya kuudhika ya kuwaza ‘vipi ikiwa,’ au kuona kwamba shida ulizo nazo ni kwa sababu ya nyumba yako yenye mzazi mmoja, au hata kwamba watoto katika nyumba zenye wazazi wawili wana maisha rahisi.”

Jambo moja ni kwamba, hata familia “iliyo bora kabisa” haikosi matatizo. Na badala ya kuona familia yako kuwa isiyo ya kawaida, waweza kuiona kuwa ugeuzi tu, jambo ambalo si baya hasa bali lililo tofauti tu. Lenye maana sawa na hiyo, ni kutoruhusu maelezo—au ukosefu wayo—ya watu wenye nia njema yaamshe maoni mabaya. Wengine, kwa mfano, huenda wakasitasita kutumia maneno kama vile “baba,” “ndoa,” “talaka,” au labda “kifo” ulipo, wakiogopa kwamba maneno hayo yatakuudhisha au kukuaibisha. Kataa kufanya vivyo hivyo. Tony mwenye umri wa miaka kumi na minne, asiyejua kamwe baba yake wa halisi, asema hivi: “Ninapokuwa karibu na wengine ambao huonekana kuzuia ulimi wao ifikapo maneno fulani, mimi huendelea na kuyatumia.” Aongeza hivi: “Nataka wajue siaibishwi na hali yangu.”

Kuziona Manufaa

Ni jambo la maana pia kuepuka kufikiri mno juu ya yale ambayo yangekuwako au yaliyokuwako. (Mhubiri 7:10) Badala yake kazia fikira juu ya sehemu zuri za maisha yako. Kwa mfano, ni yamkini kwamba mama yako apaswa kwenda kazini.a Kama tokeo, labda umepata madaraka mengi nyumbani. “Kuchukua madaraka nyumbani,” adai Melanie mwenye miaka 17, “Kunachangia kukomaa kwako haraka zaidi ya watoto wa umri wako katika familia zenye wazazi wawili, ambao huenda wakawa na madaraka machache.” Wenye ustadi hukubali hiyo. Mwanaelimu ya kijamii Robert S. Weiss wa Chuo Kikuu cha Harvard asema kwamba vijana kutoka nyumba zenye mzazi mmoja “huelekea kuwa wenye ukomavu, wenye kujitegemea,” na “wenye kujitia nidhamu zaidi.” Hizo ni sifa zenye maana, na hali yako ya kifamilia huenda ikakusaidia uzipate.

Ungeweza pia kuonea shangwe kuwa na neno zaidi katika maamuzi ya familia, kwa kuwa mara nyingi wazazi walio peke yao huona watoto wao kuwa wasiri wenye kuaminiwa. Hata hivyo, nyakati nyingine, huenda ukapaswa kumkumbusha mzazi wako kwamba ungali mchanga na kwamba ingekuwa vizuri zaidi kuzungumza mambo yenye uzito zaidi pamoja na mtu mwenye ujuzi zaidi kama vile mzee Mkristo. Bado, kuna mambo mengi mnayoweza kwa kufaa kuongea pamoja, kutia na matatizo ya kibinafsi huenda ukayakabili. Kufanya hivyo kunakusaidia kukaribia mzazi wako na kwaweza kuondoa maoni mabaya. Melanie aliyetajwa mapema, asema hivi: “Tangu talaka ya wazazi wangu, mama yangu nami twaweza kuongea kweli kweli; tumekuja kuwa marafiki wa karibu sana.”

Hiyo si kusema kwamba hutakabili matatizo. Lakini waweza kufaidika kwa kukabiliana na taabu. Biblia inasema hivi: “Ni vema mwanadamu achukue nira wakati wa ujana wake.” (Maombolezo 3:27) Kuchukua nira yako, au matatizo yenye kulemea, kwaweza kutia ndani kushughulika na taabu unazokabili katika nyumba yenye mzazi mmoja. Lakini kumbuka kwamba, hauko peke yako wakati unapochukua nira hiyo. Mfalme Daudi mwaminifu, alisema hivi: “Baba yangu na mama yangu wameniacha, bali BWANA [Yehova, NW] atanikaribisha kwake.”—Zaburi 27:10.

Hata hivyo, lenye kupendeza ni kwamba, msaada kama huo wa kimungu waweza kwa kufaa kutolewa kupitia mzazi wako anayebaki. Kwa kuitikia jitihada hizo, unaweza kukua kikawaida na kuwa na maisha ya Kikristo yenye kuthawabisha. Wayne, ambaye sasa ni mzee Mkristo, akumbuka hivi: “Nilikuwa mwenye miaka minane wakati baba yangu alipokufa, na mama alihitaji kwenda kazini. Mara nyingi alikuja nyumbani akiwa amechoka na kuishiwa nguvu. Lakini sikuzote alihakikisha tulikuwa na mafunzo ya Biblia ya familia ya kawaida na kuhudhuria mikutano ya Kikristo pamoja. Ninapokumbuka yaliyopita, naweza tu kumshukuru Yehova kwa ajili ya mama mwenye kujidhabihu kama huyo.”b

[Maelezo ya Chini]

a Zaidi ya asilimia 90 ya familia zenye mzazi mmoja katika United states zinaongozwa na akina mama.

b Makala za wakati ujao zitavumbua majaribu mengineyo yanayokabiliwa katika nyumba yenye mzazi mmoja.

[Picha katika ukurasa wa 20]

Familia yenye mzazi mmoja haipasi kutokuwa na furaha

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki