Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 6/8 kur. 9-10
  • Kitu Kingine cha Maana Sana Kuliko Pesa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitu Kingine cha Maana Sana Kuliko Pesa
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Umaana wa Hekima
  • Ni Yapi Yaliyo Mambo Yako ya Maana?
  • Tosheleza Mahitaji Yako ya Kiroho
  • Tunapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Pesa?
    Amkeni!—2007
  • Maoni Yenye Usawaziko Kuhusu Pesa
    Amkeni!—2015
  • Je, Pesa Ndio Chanzo cha Uovu Wote?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Jinsi ya Kupanga Matumizi ya Pesa
    Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 6/8 kur. 9-10

Kitu Kingine cha Maana Sana Kuliko Pesa

“Tamaa yetu mpaka leo imejengwa kabisa kwa mambo ya kifedha.”psychology Today.

NANCY na Howard walikuwa na mipango mingi baada ya kuoana katika 1989. Walitaka nyumba, mtoto, magari mapya, na likizo ya hali ya juu. Walikuwa na mapato ya kuweza mambo hayo. Lakini kwa ghafula wakajipata hawana kazi. Pesa zilizowekwa akiba kwa malipo ya kwanza ya nyumba sasa zingetumiwa kwa kulipa kodi ya nyumba.

Wakihofia wakati wao ujao, iliwalazimu kuahirisha mipango yao yote—kutia ndani ule wa kuanzisha familia. “Miaka mitano kuanzia sasa,” akasema Nancy, “sifikiri tutafikia pale tulipokuwa. Yote hayo yameenda, na sifikiri yatarudi tena kamwe.”

Jinsi jambo hilo linavyoonyesha pigo kubwa la tokeo la kupoteza kazi! Lakini pia laonyesha wazi uwezo wa pesa wa kudanganya akili. Lililopo leo laweza kutoweka kesho. Kama Biblia ionyavyo: “Pesa zako zaweza kupuruka, kana kwamba zimemea mabawa na kupuruka kabisa kama tai.”—Mithali 23:5, Today’s English version.

Ni kawaida kukubali kwa maneno kuliko kwa matendo kwamba pesa haziwezi kudumu. “Pesa ndiyo kiwango cha kipimo ulimwenguni,” lasema gazeti Psychology Today kuhusu mielekeo ya kawaida kuelekea pesa. “Tunaweka faida kwayo, hasa kwetu sisi.” Tamaa ya kupata pesa imeongoza hata wengi walio na usitawi kuwa na mahangaiko ya kudumu, mshuko wa moyo, na magonjwa mengineyo ambayo kwa ucheshi yamewekwa pamoja chini ya jina rahisi yaani mafua.

Umaana wa Hekima

Lakini kuna jambo lingine la maana sana kuliko pesa. Biblia yalionyesha hilo katika Mhubiri 7:12: “Kwa maana hekima ni ulinzi, kama vile fedha ilvyo ulinzi.” Halafu mstari huongeza uhakika wa hekima kuonyesha kwamba ni ya juu kuliko pesa: “Hekima humhifadhi yeye aliye nayo.”

Hekima hutia ndani uwezo wa kutekeleza maamuzi yanayofaa tukabiliwapo na hali zenye ushindani. Tukabiliwapo na upotevu wa kazi, maamuzi yanayofaa yatatuambia kwamba thamani ya kweli ya uhai hailinganishwi na shilingi na senti. Maamuzi yanayofaa pia yatatusaidia tusitawishe mambo ya maana kwa usawa, mahali pake.

Ni Yapi Yaliyo Mambo Yako ya Maana?

Ni nini unaloweka kwanza maishani? Je! kazi yako inastahili sana kuliko ndoa yako? Je! nyumba yako inastahili sana kuliko watoto wako? Je! pesa zastahili sana kuliko afya yako? Kila siku twafanya maamuzi yenye kutegemea tamaa yetu, mambo yetu ya kwanza. Tukabiliwapo na shida za kifedha, mambo hayo yataonyesha hatua yetu tutakayochukua. Lengo la mambo yako ya kwanza ni nini?

Yesu Kristo alisema: “Heri walio maskini wa roho.” (Mathayo 5:3) Ona kwamba Yesu alionyesha kwamba kuwa mtu wa kiroho, ni jambo linalohitajika, jambo la kutangulizwa, si sifa tu ya kufuatia wakati kila kitu katika maisha ya mtu ni sawasawa.

Ni mwito wenye ushindani kupatia nafasi ya kwanza uhitaji huo wa kiroho mtu akiwa chini ya mkazo wa kuandalia familia yake kimwili. Hata hivyo, wale hufanya hivyo, kama vile Yesu alisema, wana heri. Wakifikiria juu ya kupata mapato ya kutosha, wanakosa yale “maumivu yenye kuchoma akili yasiyoelezeka” ambayo mtu hupata akiweka pesa kwanza. (1 Timotheo 6:10, Phillips) Hao pia hupata faraja kutokana na maneno ya Daudi kama ilivyorekodiwa kwenye Zaburi 37:25: “Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa, Wala mzao wake akiomba chakula.”

Tosheleza Mahitaji Yako ya Kiroho

Uhitaji wa kiroho wa mwanadamu ni wa asili. Anahitaji zaidi ya chakula, mavazi, na makao. Mambo ya kiroho huwa zaidi yakitokeza maswali kama vile, ‘Kwa nini niko hapa?’ na, ‘Ulimwengu huu uko wapi—na maisha yangu—yanaelekea wapi?’

Woga wa “ufunuo wa kiuchumi” umesukuma wengi kuona uhitaji wao wa kiroho. Gazeti Newsweek laripoti: “Uuzaji wa vitabu vya kiunabii—vile vyenye kufasiri matukio ya karibuni kama ishara za Kibiblia za mwisho wa dunia—ni hadi asilimia 50 mpaka 70 mwaka uliopita.” Hata hivyo, ili kutosheleza uhitaji huo wa kiroho, ni lazima mtu atafute maarifa sahihi, si kisio la kibinadamu.

Tunakukaribisha ulichunguze Neno la Mungu, Biblia Takatifu. Inatoa hekima ya kukusaidia uwezane na mahangaiko ya maisha. Zaidi ya hilo, Biblia yaweza kukupatia maarifa sahihi ya maana iliyopo ya “nyakati za hatari.” (2 Timotheo 3:1) Kwa kuandikia wachapishaji wa gazeti hili, funzo la bure la Biblia laweza kupangwa. Sasa kuliko wakati mwingine wowote ndio wakati wa kutafuta hekima ya wakati huu—na maarifa sahihi ya wakati ujao—kutoka kwa neno la Mungu, Biblia.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Thamani za kiroho ni za kuhazini

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki